HII NI NIZAWADI YA AJABU KUTOKA KWA NEEMA
"Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu, wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu" (Waefeso 2:8-9, ESV).
Maisha yetu katika Kristo huanza kwa neema, inaendelea kwa neema, na itaisha kwa neema. Mara tunapofahamu jambo hili, maisha yetu yatakuwa na uhuru badala ya utumwa; kwa furaha badala ya uchovu; kwa furaha badala ya hofu. Kutumia muda mbele ya Mungu kutaonekana kama zawadi ya furaha kwa sababu tutakuja kuelewa kwamba sisi si watumishi tena lakini marafiki wa Yesu.