WAKATI MUNGU ANAKUWA KIMYA

Carter Conlon

Tunapoangalia safari yake, tunaona bilashaka Mfalme Daudi alianza kwa nguvu. Roho Mtakatifu alikuja juu yake, akimfanya kushinda simba na dubu, na hatimaye jitu Mfilisti. Ilionekana kama siyo mwisho wa kile ambacho Mungu angeenda kufanya kupitia maisha yake, mpaka wakati wa utulivu ulikuja. Ghafla Mungu hakuwa akizungumza jiya aliyotumia, na Daudi akaanza kupoteza imani. Alipoteza imani katika maneno ya zamani ya Mungu juu yake, ambayo ilimfanya ajaribu kuongoza maisha yake kwa hekima yake mwenyewe na kutatua matatizo yake kwa nguvu zake mwenyewe (angalia 1 Samweli 27:1-3).

Hatimaye wakati Daudi alifika mwisho wake, akitambua kuwa kufuata hoja yake mwenyewe tu ingemletea yeye na wengine huzuni kubwa, alirudi kwenye chemchemi ya nguvu zake (angalia 1 Samweli 30:1-3,6). Daudi alijihimiza katika Bwana, akikumbuka jinsi Mungu alikuwa kila mara mwaminifu kwake. Na katika wakati huo wa kukumbuka, alirudi kwenye sala. Sauti ya Mungu ikawa wazi tena, na Bwana hatimaye akamleta katika ushindi ambao ulikuwa nawo kila mara.

Hii inatumika kama kumbukumbu kuwa kati kati ya utulivu wa Mungu, unapaswa kupinga jaribio la kukufanya kujaribu kile ambacho Mungu alikuambia atafanya katika maisha yako. Badala yake, jihimize mwenyewe katika Bwana kama Daudi alivyofanya. Kumbuka jinsi Mungu amekuwa mwaminifu. Fikiria juu ya maneno aliyokuambia mara ya kwanza, ushindi uliopata ambao haujawahi kutokea mbali na kazi ya Roho Mtakatifu ndani yako. Ikaa chini na useme, "Mungu, umenena neno kwangu. Ninaelewa kwamba kuna muda uliowekewa hilo ili litimizwe. Jibu linakuja, na ingawa inaweza kuonekana kwamba linaweza kuwa ngumu na ahadi zako kuonekana zimezongwa na misukosuko, wewe ni Mungu asiyeweza kusema uongo!"

Carter Conlon alijiunga na jopo la wachungaji wa wa Times Square Church mwaka wa 1994 kwa mwaliko wa mchungaji muanzilishi, David Wilkerson, na alichaguliwa kuwa Mchungaji Mkuu mwaka 2001.