KUULIZA, KUTAFUTA NA KUGONGA KATIKA SALA

David Wilkerson (1931-2011)

Baadhi ya walimu wa Biblia wanasema tunatembea katika kutokuamini ikiwa tunamwomba Mungu kwa kitu kimoja mara kwa mara. Hiyo ni uzushi! Mungu ametuamuru kuuliza, kutafuta, haraka - kulia kwa sala ya kweli, kwa bidii (tazama Mathayo 7:7-8). Kutoka mwanzo, watumishi wa kweli wamegeuza ahadi za Mungu katika sala:

  • Yesu alijua Baba yake kama ameahidi vitu vyote kabla ya msingi wa ulimwengu. Hata hivyo, Kristo alitumia saa nyingi kusali ili mapenzi ya Mungu yatendeke duniani. Hata liwaambia mfano unaoonyesha kusisitiza katika sala, juu ya "mjane aliye omba lila mara" ambaye aliendelea kuomba haki kutoka kwa hakimu hadi alipoipata (Luka 18:1-8).
  • Mungu alimpa Ezekieli unabii wa ajabu juu ya marejesho ya Israeli, na kuahidi kuwa mabomo ya taifa angegeuka kama bustani ya Edeni. Tena Bwana alisema neno lake kama halingetimizwa bila sala: "Tena kwa ajili ya jambo hili ntaulizwa na nyumba ya Israeli, ili niwatendee" (Ezekieli 36:37). Kwa maneno mengine, "Nimekufanya ahadi, lakini nakutaka uombe ili lipite, nitafuteni kwa moyo wako wote mpaka ukiona Neno langu linatimizwa nami nitakuokoa, lakini kwanza lazima uulize."
  • Mungu aliahidi Danieli kwamba baada ya miaka sabini Israeli imekuwa ingerejeshwa. Wakati Danieli alipoona mwaka uliochaguliwa kufika, angeweza kusubiri kwa imani ya Mungu kutimiza neno lake. Badala yake, Danieli akaanguka kifudifudi na kuomba kwa wiki mbili mpaka alipoona Bwana alipo pitisha kila kitu (Danieli 9:24-27).

Katika Agano la Kale, Kuhani wa Israeli alibeba kwenye kifua chake majina ya kabila zote za Israeli. Hii ilikuwa inaonyesha kwamba mahitaji ya watu yaliendelea kuwa kwenye moyo wa kuhani katika sala. Ni picha nzuri sana! Inawakilisha Kristo akibeba ndani ya moyo wake na kutoa mahitaji yetu kwa Baba. Tena hiyo ndio picha ya kila Mkristo, ukuhani wa uwaminifu, kubeba mahitaji ya wengine ndani ya mioyo yetu.