KUJENGA JUU YA IMANI YETU

David Wilkerson (1931-2011)

Kama vile Daudi alivyoandika Zaburi yake, alijenga juu ya imani yake mwenyewe kwa ujuzi unaozidi kuongezeka kwa ukuu wa ajabu wa Mungu.

"Katikati ya miungu hakuna kama wewe, Bwana, wala matendo mfano wa matendo yako. . . . Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, wewe ndiye mfanya miujiza, Niwe Mungu peke yako" (86:8,10).

Kulingana na Daudi, hofu zetu zote zinaangukia katika ujuzi wa ukuu wa Mungu. Anapanua vipimo vingi vya ukuu wa Bwana wetu ili kujenga imani yetu.

"Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu, Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote. Mkononi mwake zimo bonde za dunia, Hata vilele vya milima ni vyake" (Zaburi 95:3-4).

"Yeye peke yake afanya maajabu makuu . . . Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu . . . Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji . . . Yeye aliyefanya miaanga mikubwa . . . Jua litawale mchana . . . mwezi na nyota zitawale usiku" (136:4-9).

Wanasayansi wa anga wanatuambia kama siyo mamilioni tu ya nyota, lakini mabilioni ya nyota katika ulimwengu wa juu. Wao hawana hesabu, na Mungu wetu aliumba kila mmoja. Hakika, anajua nyota kila mmoja na anawaita wote: "Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina" (147:4).

Kwa kiufupi, hatuwezi kuchukua katika maajabu mengi ya Mungu wetu. Ukuu wake unazidi ufahamu wetu!