KUTEMBEA KATIKA ROHO

David Wilkerson (1931-2011)

Mtume Paulo alisema, "Endeni kwa Roho, wala hamutatimiza kamwe tamaa za mwili" (Wagalatia 5:16). Alisema pia, "Ikiwa tunaishi katika Roho, na tuenende pia kwa Roho" (5:25).

Kutembea katika Roho ni kumruhusu Roho Mtakatifu kufanya ndani yetu kile Mungu alimtuma kufanya. Yesu alisema juu ya Baba, "Atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi milele – ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumuoni wala haumjui; lakini ninyi mnamjua, kwa maana anakaa nanyi na atakuwa ndani yenu” (Yohana 14:16-17).

KUWEZESHWA NA ROHO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Wale ambao wanashikilia imani isiyo geuka, wako kwa udhihirisho mtukufu wa nguvu ya ufufuo wa Kristo. Ni wewe na Bwana tu ndio mtajua shughuli zote za karibu lakini atakushangaza; atakufurahisha; atakuonyesha utukufu wake!

Ukuu wa sasa wa Kristo unaweza kuangaziwa kwa kifungu kimoja cha nguvu: "Ndani yake ndimo kulikuwa uzima" (Yohana 1:4) Alikuwa - na sasa - ni mwenye nguvu ya maisha. Yesu alikuwa akigeuzwa kila wakati alipokuwa akichota kwenye hifadhi ya siri ambayo haikumalizika. Yeye hakuchoka na umati wa watu ukimshinikiza na uvumilivu wake haukuvaa  kukonda.