KUWEZESHWA NA ROHO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Wale ambao wanashikilia imani isiyo geuka, wako kwa udhihirisho mtukufu wa nguvu ya ufufuo wa Kristo. Ni wewe na Bwana tu ndio mtajua shughuli zote za karibu lakini atakushangaza; atakufurahisha; atakuonyesha utukufu wake!

Ukuu wa sasa wa Kristo unaweza kuangaziwa kwa kifungu kimoja cha nguvu: "Ndani yake ndimo kulikuwa uzima" (Yohana 1:4) Alikuwa - na sasa - ni mwenye nguvu ya maisha. Yesu alikuwa akigeuzwa kila wakati alipokuwa akichota kwenye hifadhi ya siri ambayo haikumalizika. Yeye hakuchoka na umati wa watu ukimshinikiza na uvumilivu wake haukuvaa  kukonda.

Yesu alipowaita wanafunzi wake waje kando kwa muda ili wapumzike, walienda mahali pa utulivu kwenye ziwa. Umati wa watu walikuwa wakingojea hapo pia. Lakini si mara moja alisema, "O, hapana! Ndio shida tena kwa malalamiko yao ya kipumbavu na maswali bubu. Hajawahi kuaona akiisha” Badala yake, aliona umati wa watu na akawa na huruma kwa ajili yawo. Aliongezewa nguvu na Roho na akaenda kufanya kazi. Na ingawa alikuwa ni ngumu kwa mchana na  usiku kwa kuwa kwenye maombi, bado aliendelea na kuwa na wakati wa kuwa na watoto wadogo.

Katika wakati wa uchovu, Yesu alisimama ili akapumzike kando na kisima, lakini mwanamke aliyepotea alihitaji msaada na kwa mara nyingine aliongezewa nguvu. Wanafunzi wake walipata Mwalimu wao akiwa amepumuzika, nakufalijika moyoni! "Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua nyinyi" (Yohana 4:32). Hii ndiyo nguvu ya siri ya maisha ya ufufuo!

Waumini wa leo wameahidiwa maisha yaleyale ya nguvu ya Kristo. "Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo katika wafu pia atatoa uzima kwa miili yenu inayokufa kupitia Roho wake anayekaa ndani yenu" (Warumi 8:11).

Ni wazi katika maandiko kuwa Roho Mtakatifu anakaa ndani yetu kuzaa maisha ya kila wakati. Mungu ametoa nguvu yake mwenyewe kuja kwa miili yetu ya kibinadamu na kutupatia nguvu za mwili: "Na ninyi mlipokuwa mmekufaa kwa sababu ya makosa yenuna  kutotahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye" (Wakolosai 2:13).

Mshukuru Mungu kwa ukuu wa sasa wa Bwana wetu Yesu Kristo! Inafaa kwa imani na kutembea katika maisha ya ufufuo na nguvu!