WITO KWA WATU WA KAWAIDA

Carter Conlon

Moyo wangu unaimba na wazo kwamba katika historia yote ya maandishi, wakati Mungu alikuwa anataka kufanya jambo fulani kubwa, mara nyingi alimtafuta mtu ambaye ndiye aliyeweza kuifanya iweze kutokea. Wakati alitaka kuleta nabii kwa taifa, alitafuta tumbo tasa katika mwanamke anayeitwa Hana. Wakati alitaka kuwakomboa watu wake kutoka kwa mikono ya Wamidiani, alionekana kwa Gidioni - mdogo wa nyumba ya baba yake katika kabila la Manase. Wakati alitaka kutoa ahadi ya ajabu kwa mtu mmoja anayeitwa Abraham, akimwambia kwamba atakuwa na kizazi kama nyota za angani na ulimwengu wote utabarikiwa kupitia yeye, alisubiri hadi Abraham asingeweza kufanya hivyo kwa nguvu yake mwenyewe.

Baada ya Sulemani kuomba katika kukamilika kwa hekalu, Bwana alimtokea usiku na kumwambia, "Nimesikia maombi yako, na nimechagua mahali hapa kama nyumba ya dhabihu ... Ikiwa watu Wangu walioitwa kwa jina Langu watanyenyekea, na kuomba, na kutafuta uso Wangu, na ugeuka kutoka kwa njia zao mbaya; basi nitasikia kutoka mbinguni, na kuwasamehe kutoka dhambi zao na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafunguka na masikio yangu yatasikiliza maombi atayofanywa mahali hapa” (2 Nya. 7:12-15).

Ninaona kitu cha tabia ya Mungu katika kifungu hiki cha maandiko: utayari wake kututendea yale ambayo hatuwezi kufanya wenyewe. Unaona, ufalme wa Mungu ni juu ya wanaume na wanawake kuwa yote Mungu aliopanga kwa ajili yetu; kwa kushikilia vitu ambavyo haviko ndani ya ufahamu wetu wa asili kwa kuelewa ukweli ambao akili zetu za asili hazijui; na kuishi kwa uhuru ambao juhudi zozote za asili haziwezi kutuletea. Ufalme wa Mungu ni juu ya miujiza na rehema!

Bwana anasubiri watu wa kawaida kama wewe na mimi ili tugunduwe kitu kuhusu moyo wake. Kuja kwake kwa niaba ya waliopotea siku hizi na kuwa sehemu muhimu ya mpango wake wa jumla.

Carter Conlon alijiunga na jopo la wachungaji wa Kanisa la Times Square mnamo 1994 katika mwaliko wa mchungaji mwanzilishi, David Wilkerson, na aliteuliwa kuwa Mchungaji Mwandamizi mnamo 2001.