WEWE NI UJUMBE WA MAISHA UNAONEKANA KWA WOTE

David Wilkerson (1931-2011)

"Hatupotezi moyo ... bali kwa kuidhirisha iliyo kweli twajionesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu" (2 Wakorintho 4:1-2). Mtume Paulo anasema kwamba tunaitwa kuwa udhihirisho wa kweli. Kwa kweli, tunajua Yesu ni ukweli huu. Kwa hiyo, Paulo ana maana gani kwa kusema, kwa kweli, kwamba tunapaswa kuonyesha Yesu?

Udhihirisho ni "kuangaza" ambayo hufanya kitu wazi na kueleweka. Kwa hiyo, kwa kifupi, Paulo anasema tunaitwa kufanya Yesu kujulikana na kueleweka kwa watu wote. Katika kila maisha yetu, lazima iwe na mwanga wa asili na mfano wa Kristo.

Paulo anachukua dhana hii ya kuonyesha Kristo hata zaidi. Anasema sisi ni barua za Mungu kwa ulimwengu: "Nyinyi ndiye barua yetu, ilio andikwa mioni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote ... ilioandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama" (2 Wakorintho 3:2-3).

Nia ya kimwili haiwezi kuelewa mambo ya kiroho. Inayaona kuwa mapumbavu. Kwa hivyo Mungu alichagua Mwana kujulikana kwa wenyezambi waangalifu kwa njia yenye ufanisi zaidi: kwa kumfunua katika barua za kimwili-na-damu, ujumbe unaoweza kuhesabiwa na kila mtu. Hii hutokea tu kwa kazi ya Roho. Kwa wakati tunaokolewa, Roho Mtakatifu huonyesha ndani yetu mfano wa Yesu na anaendelea kuunda sanamu hii ndani yetu. Ujumbe wa Roho ni kutengeneza ndani yetu picha ya Kristo ambayo ni kweli na sahihi kwamba itakuwa kweli kuingia ndani ya fikila za watu.

Roho Mtakatifu hutimiza hili kwa kuzingatia mioyo yetu ya ukombozi na miili ya kujisalimisha na daima kutuchochea katika uwepo wa Yesu. Huko tunalazimishwa kuishi maisha takatifu.

Unapotumia muda mwingi pamoja naye, picha yake ndani yako itakua na maisha yako yatakuwa dhihirisho la nguvu la Yesu ambayo wale walio karibu nawe wataguswa na kuanza kutembea nayo.