WEKA YOTE CHINI NA USHIKILIE MUNGU KWA IMANI

David Wilkerson (1931-2011)

"Wakati Mwana wa Adamu atakapokuja, j! kwa kweli ataiona imani duniani?" (Luka 18:8). Kwa nini Yesu anauliza swali hilo? Inamaanisha ukosefu wa imani, si tu juu ya mambo ya kidunia lakini kati ya watu wa Mungu.

Imani ni mojawapo ya masuala yaliyozungumzwa zaidi kanisani. Kazi kubwa zinafanywa na miradi mikubwa iliyofanywa, yote kwa jina la imani. Kwa hiyo, Yesu anazungomzia nini hapa kwa kuwuliza, "Wakati tarumbeta ya mwisho italia, je! Nitaona imani yoyote?" Tunaona kidokezo kikubwa katika Waebrania: "Jihadharini, ndugu zangu, msiwe na yeyote kati yenu mwenye kuwa na moyo mbaya wa kutoamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai" (Waebrania 3:12).

Mojawapo ya matukio yanayojulikana zaidi ya kutoamini hupatikana katika hadithi ya Zakaria, baba wa Yohana Mbatizaji. Hapa kulikuwa na kuhani aliyejitolea, aliyemcha Mungu ambaye aliteseka kwa sababu ya sehemu moja ya kutoamini. Andiko linasema Zakaria alikuwa "mwenye haki mbele za Mungu, akiendlea katika amri zote na amri za Bwana asiye na maagizo yake bila lawama" (Luka 1:6). Alihudumu kwa uaminifu na alikuwa mtumishi aliyeheshimiwa, mwaminifu, lakini malaika Gabrieli alipokuwa akileta ujumbe kwamba angekuwa na mtoto, Zakaria alijazwa na shaka na kujitolea kwa kutoamini. Mungu hakuchulia hayo kwa mashaka yaa Zakaria na akampiga kwa kuwa kimya: "Na tazama, utakuwa bubu na usiwezi kusemaa mpaka siku ile yatakapotokea hayo , kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu; nayo yatatimizwa kwa wakati wake" (Luka 1:20).

Dhambi moja tu, iliweka Israeli nje ya Nchi ya Ahadi - kutokuamini! "Kwa nini hawakuingia? Kwa sababu ya kutokuamini kwao" (Waebrania 3:19, Living Bible). "Basi, na tufanye  bidi kuingia katika raha hilo, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi" (Waebrania 4:11).

Mungu wetu amefanya ahadi za ajabu kwa sisi, na anataka tumshikilie kwa ajili ya ahadi hizo. Ninakuhimiza kushikilia Neno lake la ajabu na kuingia katika mapumziko yake ya ahadi. Kisha maisha yako atakuwa ushahidi mkali kwa kizazi hiki.