WASAIDIZI KATIKA MAOMBI

David Wilkerson (1931-2011)

Ni mara ngapi unaombea wengine? Mara nyingi tunapomwambia mtu, "Nitakuombea," tunasahau kufanya hivyo. Au tunaomba moja kwa moja na kisha kusahau haraka kuhusu mahitaji yao.

Mtume Paulo alipata shida sana kwa kuwa aliogopa maisha yake: "Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi" (2 Wakorintho 1:8). Paulo alishiriki mahitaji yake na ndugu zake na baada ya kuokolewa, akawapongeza kutokana na msaada wao katika maombi (tazama 2 Wakorintho 1:11).

Hatujui hasa shida ya Paulo ilikuwa nini lakini 2 Wakorintho 7:5 inatoa muelekeo: "Kwa maana hata tulipokuwa tumefika makedonia miili yetu haikupata nafuu, bali tulidhika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani ya hofu." Paulo alikuwa katika hali ya uchovu wa aina fulani, labda akiumia kwa kimawazo, na kwa hakika alikuwa anahitaji msaada wa maombi.

Waumini wengi leo wanateseka kama Paulo alivyofanya; Maumivu yao makubwa ni ya kihisia, labda yanayosababishwa na wale waliopenda au kusaidia zaidi. Somo muhimu Paulo alijifunza katika uchungu wake ni kwamba ilikuwa ni kumugeukia Bwana. Hangeweza tena kuvumilia kwa kuamini katika mwili, uwezo wake au uwezo nguvu zake. "Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu" (2 Wakorintho 1:9).

Mzee mzuri aliandika akiniambia kwamba Mungu amemuomba aniombee kila siku na aliniuliza kama angeweza kuniweka kwenye orodha yake ya sala - ambayo ilikuwa na wajane, maskini, watumishi na watu wasiookoka. Aliongoza maisha rahisi na kuomba kwa urahisi. Ninaamini kwamba wale ambao wanaombea kwa wengine hupokea thawabu maalum sana mbinguni. Ninapofikiria juu ya roho Mungu ameruhusu kwa wainjilisti kuvuna katika ufalme, mara moja nadhani kuhusu maombi ya ajabu ya kusaidia watu kama hii mtakatifu mpendwa.