"WAMEKUWA PAMOJA NA YESU!"

David Wilkerson (1931-2011)

Muda mfupi baada ya ufufuo wa Yesu, Petro na Yohana walikutana na mwombaji aliyepooza nje ya lango la hekalu ambako walikuwa wakiabudu. Mtu huyu alipelekwa lango kila siku ili kufanya maisha yake kwa kuomba na akamwuliza Petro na Yohana kwa sadaka. Petro akasema, "Mimi sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho ikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende" (Matendo 3:6). Mtu huyo aliponywa mara moja na kwa furaha kubwa alianza mbio kupitia hekaluni, akiruka na kupiga kelele, "Yesu aliniponya!"

Watu walimtambua mulemavu, na umati wa watu walikusanyika walipokuwa nakushangaa wanayo yaona. Petro na Yohana walitumia nafasi hiyo na wakaanza kuhubiri kwa ujasiri, na kusababisha wokovu wa maelfu (tazama Matendo 4:4). Wakati wakuu wa sinagogi walipokuwa wakiona yaliyotokea, walikuwa wakikasirika na kuwapeleka wanaume hao jela. Kisha wakaomba kujua, "Kwa nguvu gani na kwa jina la nani ninyi mmefanya haya?" (4:7). Bila shaka, walijua hasa jina lao linalohubiriwa, lakini kwa makusudi walijifanya kuwa vipofu kwa hilo.

Petro akihimizwa na Roho Mtakatifu, na akajibu watawala, "Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyi mlimsululisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu ... Kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbinguni walilopewa wanadamu litunapasalo sisi kuokolewa" (4:10 na 12). Watawala walishituka na "wakashangaa. Na waligundua kwamba walikuwa pamoja na Yesu" (4:13).

Ni alama gani iliyotafautisha kati ya Petro na Yohana? Ilikuwa uwepo wa Yesu! Wakuu wa sinagogi walitambua, "Tulisulubisha Yesu, lakini bado anasema leo kwa njia ya watu hawa wawili. "Wakati huo huo, Petro na Yohana walikuwa wakitimiza amri ya Yesu ya kushuhudia juu yake "Yerusalemu" (Matendo 1:8). Vivyo hivyo, naamini ushahidi wa nguvu wa Mungu katika siku hizi za mwisho hautakuja kwa kuhubiri peke yake. Pia itakuja kupitia wanaume na wanawake ambao "wamekuwa pamoja na Yesu" kwa kujifungnia na yeye na kumtafuta kwa moyo wao wote na roho zao zote.

Ni ushahidi gani mkubwa zaidi wa Mungu ambao unaweza kuwapo kuliko maisha yaliyobadilishwa na nguvu zisizo za kawaida ya Kristo? Imeandikwa juu yenu, "Mwanaume huyo au mwanamke huyo, amekuwa pamoja na Yesu!"