UWEPO WA YESU NDANI YETU

Gary Wilkerson

Agano jipya linasisimua sana - linatuonyesha kwamba Yesu ndiye uwakilishi halisi wa Baba na wakati tunamwona Yesu, tunaona hasa jinsi Mungu alivyo. Ni mwenye kujaa upendo, neema, huruma, nguvu, kweli na haki! Neno la Mungu linatuambia kwamba tumechukua asili yake ya kimungu kwa sababu ya uwepo wa Yesu ndani yetu.

"Kwa kuwa uwezo wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utukubutauwa, kwa kumujua yeye aliyetuita kwa  utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa" (2 Petro 1:3-4).

Je! unaweza kufikiria kuishi maisha bila kuwa na hofu au kuwa na woga usiku? Au aibu, hatia, hukumu, au hisia za kutostahili? Je! Maisha yako ingekuwa kama aje bila shida au wasiwasi? Fikiria tu - na kisha ujue ukweli kwamba wewe ni huru kutoka kwa utumwa wa mambo haya kwa sababu ya wewe uko ndani ya Kristo.

Tuna maana ya kuishi kama Yesu. Tunapofanya dhambi, huvunja moyo wa Baba, bila shaka, lakini Roho Mtakatifu anatuhukumu na tunapotubu, Yesu anatukomboa na kuvunja kila ufungwa! Hatuwezi kutembea katika ushindi kila wakati wote, lakini "Tunaendelea kushinda tuzo" kwa sababu Yesu anaishi ndani yetu kwa nguvu za Roho Mtakatifu.

"Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yalio nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu" (Wafilipi 3:12-14).