UTEGEMEZI KAMILI JUU YA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Tunajua kwamba Mungu aliwaokoa Israeli kabisa. Katika kijiti cha moto, Musa alikuwa akiandaliwa kumwamini Mungu kuleta kazi hiyo ya utukufu. Angejifunza kitu kuhusu asili ya Mungu ambayo baadaye itamsaidia kumtegemea Bwana kuifanya yote. Nini kipengele hicho cha asili ya Mungu? Utakatifu wake!

Vile vile ni kweli kwa kila Mkristo leo. Tunajaribu kukamilisha katika mwili kitu tunachofikiri kwamba Mungu anataka. Lakini Bwana anatuambia kama alivyomwambia Musa, "Kuna ardhi moja tu ambayo unaweza kunishuhudia, na hiyo ni ardhi takatifu. Huwezi kuweka imani yoyote katika mwili wako, kwa sababu hakuna muili utasimama mbele yangu. Madhumuni yangu hayakujazwa na kile unachoweza kuita ndani yako mwenyewe."

Kwa hiyo, kwa nini Mungu alimwambia Musa kuondoa viatu vyake? (Angalia Kutoka 3:5). Bwana alikuwa akitumia kitu cha kawaida cha kila siku kufundisha ukweli wa kiroho, kama Yesu alivyofanya kwa kutumia sarafu, lulu, ngamia na mbegu za haradali. Mungu alikuwa akisema, "Musa, unapaswa kuvaa vazi za kinga ili kuzuia miguu yako lakini hakuna kiasi cha ulinzi wa kimwili kinachoweza kukusimamia mahari ninakutuma. Utahitaji muujiza wa ukombozi.

"Ninakutuma Misri, kukabiliana na dikiteta mgumu. Utakuwa katika hali ambayo mimi tu naweza kukuokoa. Kwa hiyo, weka kando mahitaji ya mwili wako, hata upole wako na unyenyekevu. Vinginevyo, wewe hutaweza kufanya kile ninachokuitia ufanye. Uwezo wako wote hautakuwa na maana isipokuwa nikiutakasa. Weka imani yako kamili kwa jina langu na kwa nguvu."

Hakuna mtu anayeweza kufikia utakatifu machoni pa Mungu kwa uwezo wake mwenyewe au uwezo wake. Hatuwezi kumtumikia Bwana vizuri bila kuchukua njia iliyoelezea Musa. Tunapaswa kuja kwa Mungu kusema, "Bwana, mimi sina chochote cha kukupa. Unahitaji kufanya yote."