USHINDI JUU YA USHINDI

Gary Wilkerson

Wakristo wengi wanapigana na vizuizi vikubwa katika maisha yao. Inaweza kuwa upotezaji wa kazi, ndoa yenye mkazo, mpendwa amabaye ni mgonjwa, au mtoto anayepambana na imani. Lakini haijalishi mambo yanaweza kuonekana mabaya, Mungu yuko katikati ya maisha ya wale wanaompenda na wanaomwamini.

Katika bibilia tunasoma ya mjane maskini ambaye alikuwa katika hali ya kutamani. Baada ya kifo cha mumewe, hakuweza kulipa deni lake na mdai alikuwa amekuja kumuita. Katika siku hizo, wadai hawakuchukua mali yako tu; walichukua watoto wako pia. Katika kukata tamaa kwake, mjane huyo alimwomba nabii Elisha msaada.

"Basi mke wa mmoja wa manabii alimlilia Elisha, akasema Mtumishi wako, mume wangu amekufa; na unajua kuwa mtumwa wako alikuwa mcha BWANA, lakini mdai huyo amekuja kuchukua watoto wangu wawili kuwa watumwa wake." (2 Wafalme 4:1).

Elisha angemwambia aende hekaluni kwa msaada, lakini yeye mwenyewe alichukua hatua. Nifanye nini? Niambie; una nini ndani ya nyumba?” (4:2). Kwa kweli, Elisha alikuwa akimwambia, "Mungu anaweza kukutana nawe kama ulivyo, kwa hali uliyonayo sasa. Ikiwa unayo imani, anaweza kukuzidisha hata kitu kidogo kama unayo. "Alikuwa na chupa moja tu la mafuta, lakini kwa kujibu utii wake na imani, mafuta yaliongezeka na mahitaji yake mengi zaidi ya kajibiwa kwa utukufu wa Mungu. Kwa kweli, alikuwa na usambazaji wa mafuta usio na mwisho na pia alikuwa na ushuhuda wenye nguvu kwa majirani zake. (Soma hadithi kamili katika 2 Wafalme 4:1-7.)

Bwana alitumia njia zisizo za kawaida kutowa mahitaji ya mjane huyu lakini huo ndio uzuri wa jinsi Mungu anavyofanya kazi. Mipango yake kawaida huwa juu ya kitu chochote tunachoweza kufikiria. Yeye huenda zaidi ya uwezo wetu wa kibinadamu, na anatupatia ushindi juu ya ushindi.

Haijalishi hali yako, imani yako itaendelea kukuleta mahali pa kupumzika katika Baba yako mwenye upendo. Nguvu zote za mbinguni ziko kwake na yeye anakuletea ushindi sasa hivi!