USALAMA KATIKA UPENDO WA BWANA

David Wilkerson (1931-2011)

Wakristo wengi huzungumzia kuhusu urafiki na Bwana, kuhusu kutembea pamoja naye, kumjua, kuwa na ushirika naye. Lakini hatuwezi kuwa na ushirika wa kweli pamoja na Mungu isipokuwa tukipokea ndani ya mioyo yetu ufunuo kamili wa upendo wake, neema na huruma.

Kushirikina na Mungu kuna mambo mawili: kupokea upendo wa Baba na kumpenda akirudisha. Kuwa salama katika upendo wake ni hatua ya kwanza. Unaweza kutumia masaa mengi kila siku katika sala ukimwambia Bwana kiasi gani unampenda, lakini ikiwa haujapata upendo wake, hujawasiliana naye.

Mtunga-zaburi anatuhimiza: "Ingieni milango mwake [Mungu] kwa shukuru; nyuani mwake kwa kusifu" (Zaburi 100:4). Anaendelea kutuonyesha aina ya Mungu tunaomfuata: "Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; rehema zake nizamilele; na uaminifu wake ni kwa vizazi na vizazi" (mstari wa 5).

Wengi wanaonekana mbele ya Mungu kama kielelezo kinachohitajika na sura yenye hasira tu ya kutusubiri tushindwe, ili aweze kusema, "Nimekushika wewe!" Lakini Baba yetu wa mbinguni amejifunua kuwa mwenye fadhili, mwenye huruma, mwenye kujaa neema na huruma, mwenye kuwa na wasiwasi za kuinua mahitaji yetu yote na mizigo yetu.

Nabii Zefania anaandika juu ya upendo wa ajabu wa Mungu kuhusu sisi: "Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Shujaa Awezaye kuokoa; atakushangilia kwa furaha kuu, atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba" (3:17).

Unaweza kuja katika ikuru zake kwa sifa na shukrani kwa sababu unashukuru kwa uepo wa Mungu. Licha ya udhaifu wako wote na kushindwa kwako, Baba yako wa mbinguni anajali juu ya kila kitu unachopitia.

Usiishi kwa hofu na kukata tamaa, kwa kigogo au kutokua na matumaini. Omba Bwana akusaidiye kuelewa ukweli wa upendo wake kwako na kushikilia upendo huo kwa imani.