UPENDO USIOBADILIKA WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Ushirika na Mungu una vitu viwili: kupokea upendo wa Baba na kumpenda kwa kurudi. Unaweza kutumia masaa kila siku katika maombi, ukimwambia Bwana ni kiasi gani unampenda, lakini sio ushirika isipokuwa ukipokea upendo wake.

Mtunga zaburi anatuhimiza "kuingia katika malango wake na shukrani, na kuingia katika baraza lake na sifa" (Zaburi 100:4). Kwa nini tunapewa mwaliko wa ujasiri na ni nini sababu ya kushukuru na kutoa sifa? Ni kwa sababu tumeonyeshwa aina ya Mungu tutakayokuja: "Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema yake ni ya milele, Na ukweli wake ni wa vizazi vyote” (100:5).

Mungu haji kwetu kama baba mgumu na anayedai. Badala yake, yeye ni mkarimu na mwenye moyo mpole, amejawa na upendo na rehema kwetu. Upendo wake hauna masharti na hatatukataa wakati tutamwomba. Anajali kila kitu kuhusu sisi lakini Wakristo wachache sana wameshikilia upendo na neema hii ya ajabu. Wanaishi kwa hofu na mashaka, na tumaini kidogo au hakuna.

Upendo wa kweli unaonyeshwa katika vitu viwili: kupumzika na kufurahi. Nabii Sefania anaandika: “Bwana, Mungu wako, aliye katikati yako, Yeye ni shujaa, ataokoa; Atakushangilia kwa furaha, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba" (Sefania 3:17).

Mungu anakaa katika upendo wake kwa watu wake. Kwa Kiebrania, msitali "Atakutuliza na upendo wake" inasomwa, "Atakaa kimya kwa sababu ya upendo wake." Mungu anasema, kwa asili, "Nimepata mapenzi yangu ya kweli na sio lazima nitaangalia mahali pengine."

Mungu anapata furaha kubwa kutoka kwa watu wake. Sefania anashuhudia kwamba upendo wa Mungu kwako ni mkubwa sana kwamba huweka wimbo kwenye midomo yake! 'Kufurahi' kunamaanisha kuwa na furaha na kufurahi; ni ishara ya nje ya furaha ya ndani. Pia ni usemi wa juu zaidi wa upendo.

Mungu aliona dhambi zako zote na mapungufu yako, lakini bado alikupenda upendo mpole. Ikiwa Mungu alikukupenda vya kutosha na kutowa Mwanae peke ili afe kwa sababu ya wewe wakati ulikuwa ndani ya dhambi kubwa, je! Angeondoa mapenzi yake wakati ukijikwaa au kushindwa? Sio kabisa! Upendo wake ni mtukufu na thabiti - usiobadilika na wa milele.

Tags