UJUMBE MKUBWA KATIKA MAISHA

Nicky Cruz

Familia za leo - zote za Kikristo na zisizo za Kikristo - ziko chini ya shinikizo kubwa la kujifananisha maoni ya kijamii. Wote wazazi na watoto wanapigana chini ya matatizo ya kicha cha ulimwengu na dhambi na majaribu. Wakati mwingine inaonekana tunapigana vita kwa kushikilia upande mmoja, kaa katika vita, pambana juu ya uaminifu wa familia - na pigana juu ya roho za watoto wetu.

Kitu kikubwa ambacho mzazi anaweza kufanya kwa watoto wake ni kuwaongoza katika uhusiano na Yesu na kisha kuwashauri katika imani yao. Bila Yesu, watoto wetu wameachwa bila msingi wa kujenga, hakuna kipimo cha haki na kibaya, hakuna maana halisi ya maisha yao. Wanalazimishwa kuangalia ulimwengu kwa mfumo wao wa thamani, na ulimwengu daima huja kwa ufupi.

Kuna jibu kwa matatizo ya utamaduni wetu. Kuna njia ya kukomesha vurugu na kutokuwa na tamaa kwa kila nyumba, shule, na majirani. Tunaweza kufanya hivyo kwa kuleta tena familia kuwa pamoja, na kuwawonyesha nguvu na utu wa Yesu - kwa kuita nguvu za Roho Mtakatifu wa Mungu ili kukomboa zamani zetu na kurekebisha maisha yetu ya baadaye.

Wazazi, munaweza kuwafundisha watoto wenu kuhusu huduma katika ufalme, kama askari katika vita dhidi ya umasikini wa kiroho. Kujenga juu ya msingi wa Yesu husababisha hisia ya matumaini na kusudi ndani ya familia. Wakati watoto wanapompenda sana Yesu na kumruhusu kuwatia ndani hisia ya shauku na kuamua kumtumikia, hawatakuwa muda wa uasi wakati wa ujana wao. Watakuwa na ujumbe mkubwa katika maisha.

"Nami nitawapa moyo mmoja, nitatia roho mpya ndani yao; Nitauondoa moyo wa kijiwe kutoka miili yao na kuwapa moyo wa nyama. Kisha watafuata amri zangu, na kuwa makini kwa kuweka sheria zangu. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao" (Ezekieli 11:19-20).

Nicky Cruz, mwinjilisti wa kimataifa aliyejulikana, na mwandishi mkubwa, alimgeukia Yesu Kristo kutoka kwenye maisha ya vurugu na uhalifu baada ya kukutana na David Wilkerson huko New York City mwaka 1958. Hadithi yenye kushangaza ya kuokoka kwake ilisemwa mara ya kwanza katika Musaraba na Kisu kinachomoka (Cross and Switchblade) na David Wilkerson na kisha baadaye katika kitabu chake chenye kuuzwa vizuri zaidi, kiitwaco: Kimbiya, Mtoto, Kimbiya (Run, Baby, Run).