UHUSIANO WA INJILI

Gary Wilkerson

Ninapenda maneno ya nyimbo ya zamani tulikuwa tukiimba, "Nani kama ndugu tunao ndani ya Yesu, anabeba dhambi zetu zote na maumivu yetu! Ni fursa ya kubeba kila kitu kwa Mungu kwa sala "(Joseph M. Scriven). "Mtu ambaye ana marafiki lazima awe mwenye kuwa na urafiki, lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu" (Methali 18:24).

Mungu aliongeza ukamilifu wa upendo wake kwetu kwa njia ya zawadi ya Mwanawe: "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu sana, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" (Yohana 3:16). Na kwa sababu ya upendo wake mkubwa kwetu, tunawezeshwa kuwafikia wengine kwa njia za upendo.

Sisi sote tunataka mtu katika maisha yetu ambaye anashirikisha maadili na viwango vyetu, rafiki ambaye atakuwa mwaminifu na anatupenda licha ya udhaifu wetu. Tunasoma juu ya urafiki wa aina hiyo katika 1 Samweli 18:1, 3-4: "Roho ya Yonathani iliunganishwa na roho ya Daudi, na Yonathani akammpenda kama roho yake mwenyewe." Ndipo Yonathani akafanya agano na Daudi, kwa sababu alimpenda yeye kama nafsi yake mwenyewe. Naye Yonathani akajivua vazi lake, akampa Daudi, na silaha zake, na hata upanga wake, na upinde wake, na ukanda wake.

Aya hizi zinawakilisha upendo ambao Yesu anao kwa ajili yetu - upendo sisi usio tufaa, usio wa kawaida, upendo unaoona mbali udhaifu wetu na unaendelea kusaidia na kuhimiza. Unaitwa agape upendo wa Mungu na ni juu ya ufahamu wa binadamu. Aina ya urafiki wa upendo ambao Jonathan na Daudi walichangia - Ninaiita ya uhusiano wa injili - unaweza kuja tu kupitia nguvu za Yesu Kristo.

Kwa kuwa unapokea zawadi hii ya upendo kutoka kwa Yesu kwa uhuru, kumwomba kunakuwezesha kuwa rafiki wa kiMungu ambaye huhimiza ukuaji wa kiroho kwa mtu mwingine - kweli "rafiki anayekaribia karibu kuliko ndugu."