UHURU KUTOKA KWA NGUVU ZA DHAMBI

David Wilkerson (1931-2011)

Mengi yameandikwa juu ya asili ya dhambi: dhambi ilitoka wapi? Tuliambukizwaje na hiyo? Nini kuhusu ushiriki wa Lucifa katika uasi dhidi ya Mungu? Je! Dhambi iliwasiliana kutoka kwa Adam hadi kwa watu wengine?

Roho Mtakatifu anataka kutuonyesha jinsi ya kushughulika kwa uaminifu maovu yaliyopo sasa ndani yetu ... asili yetu ya dhambi. Paulo alifanya ugunduzi ambao umemfanya afurahi na kusema, " Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio ‘katika’ Kristo Yesu. Kwa sababu sharia ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sharia ya dhambi na mauti." (Waroma 8: 1-2, Phillips). Anazungumzia kuhusu kanuni mpya za uzima ndani ya Yesu ambazo zimezuia dhambi inayofurahisha-kwenda-pande zote, akawondoa mwendo usiyo na mwisho, na kumfungua mara moja tu kutoka kwa nguvu zake.

Mojawapo ya kanuni mpya Paulo alizozungumzia ni kwamba waumini hawako watumwa wa dhambi. Hatuna wajibu wa asili yetu ya kimwili (tazama Warumi 8:12, Phillips). Abraham Lincoln anasemekana kuwa "amewapatia uhuru watumwa" na Tangazo la Kuwa huru kuto utumwani liliyotolewa Januari 1, 1862. Hati hii ya kisheria ilitangaza kuwa wutumwa umekufa ... na watumwa walipatiwa uhuru!

Inawezakana kusikika vizuri sana kwa kuwa kweli, lakini Kristo aliwapatia uhuru watumwa wote wa dhambi huko Kalvari. Wote wanaweza kutupa mzigo wao wa dhambi, kwa kukimbia mbali kutoka utawala wa Shetani, na kuingia katika maisha mapya ya uhuru. Biblia inasema, "Kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi" (Warumi 6:7-8). Kinachomaanisha ni kwa kuwa suala la utumwa wako wa dhambi ni suala lilo kufa, kwa kuwa Kristo amekwisha kutangaza kwamba uko huru, sasa uko huru kwa kuishi kama mtu mpya katika Kristo - uliofunguliwa.

"Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru" (Yohana 8:36). Wakati Biblia inasema sisi tuko huru kutoka kwa dhambi, hakuna hoja tena. Suala hilo haliwezi kuzingatiwa! Tembeya ndani ya ushindi leo kwa kujua kwamba wewe uko huru kutoka kwa dhambi na kifo kwa sababu ya Kristo.