TUTAMUONA YESU

David Wilkerson (1931-2011)

Mbinguni! Ahadi ya mbinguni ni msingi wa injili, lakini hatusikii mengi juu ya somo hili la furaha siku hizi. Kwa kweli, Biblia haisemi mengi kuhusu mbingu inavyofanana. Yesu hakuketi pamoja na wanafunzi na kuelezea utukufu na heshima vya mbinguni. Alimwambia mwizi msalabani, "Leo utakuwa pamoja nami katika Paradiso," lakini hakuielezea (Luka 23:43).

Katika 2 Wakorintho 12: 1-6, mtume Paulo anaelezea mbinguni wakati anaposema juu ya kupelekwa kwenye Paradiso. Anasema aliona na kusikia vitu ambavyo vilikuwa vyenye kumuzidia akili sana, hakuwa na lugha ya kuelezea hilo. Ingawa alikuwa ikitowa shukrani kwa maisha yake na wito wake, katika miaka mingi yake yote ya huduma, hamu yake ya kuendelea ilikuwa kwenda nyumbani na kuwa pamoja na Bwana. Alinena kwa uwazi juu ya hamu yake ya mbinguni alipoandika, "Tuna hakika, ndiyo, nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana" (2 Wakorintho 5:8).

Tunajua kwamba kiti cha enzi cha Mungu kiko mbinguni na Yesu yuko pale pamoja na malaika katika makundi mengi. Paulo anasema kwamba wakati tutakuwa pale, tutamwona Yesu "uso kwa uso" (1 Wakorintho 13:12). Tunakwenda kuwa na hapo napo wa kibinafsi unaotuwezesha kufika kwa Bwana milele na milele, na ukweli huo pekee unapaswa kufanya mioyo yetu ifurahi. Yesu amekwenda kutuandalia makao ambapo tutaishi pamoja naye milele (ona Yohana 14:3).

Hatutakuwa na kupumzika kidogo na "kuwa na kanisa" wakati wote mbinguni. Biblia inatuambia kwamba tutatawala pamoja na Bwana kama "wafalme na makuhani kwa Mungu wetu" (Ufunuo 5:10). Pia, tutapewa kazi za kusisimua katika ulimwengu huu mpya na tutatenda kama watumishi wake (angalia Ufunuo 22:3). Hakutakuwa na machozi mbinguni: "Mungu atafuta kila machozi katika macho yao" (21:4). Hakuna huzuni, hakuna maumivu, hakuna kifo, hakuna hofu.

Wapendwa, fanya mbingu kuwa tamaa yako kubwa. Yesu anakuja kwa wale wanaotamani kuwa pamoja naye hapo!