TAFUTA UONGOZI WA MUNGU

Nicky Cruz

Nilikuwa na myaka ishirini na mbili tu wakati Mungu aliweka moyoni mwangu mapenzi yake kwangu kuwa mhubiri. Aliniagiza kutumia historia yangu na ushuhuda wangu wa kusukuma wenye dhambi kwa wokovu, na tangu wakati huo nimebakia mwaminifu kwa wito huo. Wakati mwingine nimekuwa nimechoka kwa kuwaambia hadithi yangu, na nilipendelea Mungu anitumie kwa lengo lingine. Ni vigumu kufikisha kumbukumbu mara kwa mara.

Mara nyingi nimejiuliza, "Je, ni madhara gani ikiwa ningeingia kwenye mstari mwingine wa huduma? Labda ningeweza kuchunga kanisa au kuweka semina juu ya masuala ya ndoa na familia - kitu ambacho kitanihusu nitumie zaidi zawadi na vipaji vyangu. Au labda ningeweza kwenda biashara!"

Lakini basi ninakumbuka wito wangu, na mawazo hayo yanapungua haraka. Hakuna chochote kibaya na yoyote ya fani hizi; sio tu kile ambacho Mungu alikusudia maisha yangu. Mimi ni mwinjilisti, balozi wa neema ya Mungu na msamaha. Ninawaambia watu kuhusu Yesu na kuwaongoza kwenye wokovu mbele ya kiti chake cha enzi. Hiyo ndio kusudi langu mbele za Mungu pamoja na zawadi yangu ya kiroho. Wakati Mungu alinipa wito huu, hakunipa tu uwezo wa kuichukua, lakini aliweka moyoni mwangu huruma kwa waliopotea. Alinipa macho ili kuona wazi watu wanaohitaji msamaha, kisha akaniweka kwenye njia ya kuwapata. Na kwa sababu nimejaribu kubaki kuwa mkweli kwa maono hayo, ameweza kunitumia mimi kwa utukufu wake. Gloria, mke wangu, daima amehisi wito huo huo juu ya maisha yake.

Unaweza kuwa na wito mwingine na taaluma. Mungu ameumba kila mmoja wetu na talanta na karama tofauti - lakini sisi sote tunaitwa kufikia waliopotea! Tunapaswa kutafuta mwongozo wake na maono kwa maisha yetu na kisha tuendelee kuzingatia na kujitolea kwa sababu hiyo.     

Nicky Cruz, mwinjilisti wa kimataifa aliyejulikana na mwandishi mkubwa, alimgeukia Yesu Kristo kutoka kwenye maisha ya vurugu na uhalifu baada ya kukutana na David Wilkerson huko New York City mwaka 1958. Hadithi yenye kushangaza ya kuokoka kwake ilisemwa mara ya kwanza katika Musaraba na Kisu kinachomoka ( Cross and Switchblade) na David Wilkerson na kisha baadaye katika kitabu chake chenye kuuzwa vizuri zaidi, kiitwaco:Kimbiya , Mtoto, Kimbiya (Run, Baby, Run).