SIRI YA UMOJA

David Wilkerson (1931-2011)

Katika Yohana 13, Yesu alichukua kitambaa na baseni na kuosha miguu ya wanafunzi wake.

"Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa nyinyi" (Yohana 13:14). Baada ya kuwatawadha miguu yao, akawauliza, "Je, mnajua kile nilichowafanyia?" Kwa maneno mengine, "Je, munaelewa maana ya kiroho ya kutawadhana miguu?"

Ninaamini wakati Yesu alitawaza miguu ya wanafunzi, alikuwa akifundisha somo la kina juu ya jinsi ya kupata umoja wa ushirika ndani ya Mwili wa Kristo.

Yesu alipomkaribia Petro amutawadhe miguu, mwanafunzi huyo alishangaa tena. "Bwana, huwezi kutawadha miguu yangu kamwe!"

Yesu akamjibu, "Kama nisipokutawadha, huna shirika nami" (Yohana 13:8). Yesu alikuwa akisema, kwa kweli, "Petro, ikiwa ninatawadha miguu yako, tuna sababu za ushirika, msingi wa umoja wa kweli." Anawataka watoto wake watumike na kujisalimisha kwa nyumba ya Mungu.

Je! Yesu alikufanyia nini wakati alipokutakasa? Aliifuta hatia yako yote na ukafanywa safi, na kuwa mzima. Anaweka shukrani na furaha katika roho yako. Alikujaza kwa upendo kama huo kwa kuwa unamfuata kila mahali na kumfanyia chochote. Yote uliyotaka ilikuwa ushirika naye kwa sababu ya kile alichokufanyia.

Wapendwa, hiyo ndiyo siri ya umoja. Unapochukua kitambaa cha rehema kwa ndugu anayeumizwa, aliyeanguka, unamtia moyo kwa kumkumbatia katika kuumizwa kwake - kwa kuwasilisha hofu ya kimungu, kuosha hisia zake za kutokuwa na maana, shida na kukata tamaa, kwa kumpenda na kumtunza.

Je! Umefanya nini kwa mtu huyo kwa kutawaza miguu yake, iwe ni kwa kiroho au kimwili? Umejenga msingi wenye nguvu wa umoja wenye kweli na ushirika wa utukufu. Wewe ni mmoja kwa uzoefu wako wa kawaida - yaani, kwa kutawazwa na maji ya Neno.