SHIDA ZAKO SI KUBWA KULIKO NEEMA YA MUNGU​

Gary Wilkerson

Hatuwezi kuelewa Injili isipokuwa tunajua hali ya utukufu wa Mungu wetu wa kutisha. "Macho  ya mioyo yenu yatiwe nuru, ili nanyi mjue" (Waefeso 1:18).

Injili haiwezi kuanza kwa kutambua kuwa wewe ni mwenye dhambi au kutambua kwamba Mungu ana mpango mzuri wa maisha yako. Inaanzia kwa kuelewa neema ya Baba yetu mwenye utukufu.

Kuwa katika mbele ya Bwana huangazia uelewa wetu na kweli ni kwamba imevunjika mbele ya Mungu wetu mzuri saana kuziti yote na mwenye nguvu. Paulo anasema hapa, "Nataka macho yako kuwa wazi kwa ukweli wa tabia ya Mungu huyu mzuri ambaye tunamtumikia. Yeye si mdogo, mdogo sana, au mwenye kutofaa. Yeye ndiye Mungu mmoja, wa kweli, na anataka tuwe macho yenye kuwa wazi kwa ufunuo wa asili yake."

Musa alikuwa na njaa na kiu vya kujua ni nani Mungu - jinsi asili yake na tabia yake zilivyokuwa - na akasema, "Nakusihi unioneshe utukufu wako!" (Kutoka 33:18). Lakini Musa hakuwa na uwezo wa kuona uso wa Mungu kwa sababu alikuwa mbali sana na utukufu. Badala yake, Mungu alikuja kwake kwa ufunuo rahisi: "Bwana alipita mbele yake na kutangaza," Bwana, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhali, mwepesi wa hasira, na mwingi wa rehema na kweli, mwenye kusamehe uovu na uasi na dhambi" (34:6-7).

Omba ili Mungu akufungue macho ili uweze kujua "mjue tumaini la mwito wake jinsi ulivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo , kwa kadiri ya utendaji wa nguvu uweza wake" (Waefeso 1:18-19).

Fikiria ukuu mkubwa usiokuwa na kipimo wa Mungu. Usifikiri kwamba matatizo yako ni makubwa zaidi kuliko uwezo wa Mungu wa kuyatatua. Wala usifikiri kwamba mapambano yako ya kimwili ni makubwa kuliko uwezo wake wa kushinda. Na kama unatambua ukuu wake, towa shukrani na utukuza jina la Bwana kwa yote aliyokufanyia kwa sababu ya neema yake ya ajabu.