ROHO MTAKATIFU, MWARIMU WETU

David Wilkerson (1931-2011)

Ikiwa moyo wako unahamasishwa na idhini ya wengine na hii inaathiri njia unayoishi, uaminifu wako umegawanyika. Utakuwa daima unajitahidi kumpendeza mtu mwingine kuzidi Yesu.

Miaka michache baada ya mtume Paulo kugeuka, alienda katika kanisa la huko Yerusalemu ili kujaribu kujiunga na wanafunzi huko. "Nao walikuwa wakimwogopa wote, wasisadiki ya kuwa yeye ni mwanafunzi" (Matendo 9:26).

Mitume walijua sifa ya Paulo kama mtesaji. Makanisa ya Yudea yaliyasikia tu kwamba, "Huyo aliyotuuzi hapo kwanza, sasa anaihubiri imani ile aliyoiharibu zamani" (Wagalatia 1:23). Lakini Barnaba aliwasaidia mitume kuushinda uoga kuhusu Paulo na wakampa ushirika. Paulo aliamua kusafiri kati ya Wayahudi na alikuwa makini kuelezea wito wake waziwazi, akielezea kwamba haikutoka kwa wanadamu wala kwa njia ya mwanadamu, "bali kwa njia ya Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka wafu" (Wagalatia 1:1).

Kisha Paulo aliongeza kwa uwazi, "Kwa maana, ndugu zangu, injili hiyo niliowahubiri nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu. Kwa maana mimi sikuipokea kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mwanadamu, bali alikuja kwa ufunuo wa Yesu Kristo. . . . Mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu" (Wagalatia 1:11-12, 16).

Kitu Paulo anasema hapa kinatumika kwa wote wanaotaka kuwa na mawazo ya Kristo: "Sikuhitaji kusoma vitabu au kukopa njia za watu ili nipate kile nilicho nacho. Nilipokea ujumbe wangu, huduma yangu na upako wangu juu ya magoti yangu.

"Mambo haya yalikuja nilipofungwa na Bwana, kuomba na kufunga. Ufunuo wowote wa Kristo umekuja kutoka kwa Roho Mtakatifu, anayeishi ndani yangu na anaongoza maisha yangu. Siwezi kuruhusu mwenyewe kufuata mwenendo na vifaa vya wengine."

Paulo alikuwa si mhubiri mwenye kujivuna na kujisifu. Alijitoa kwa nafsi yake mwenyewe, na aliruhusu Roho Mtakatifu awe mwalimu wake!