NJIA YA KUEPUKIA

David Wilkerson (1931-2011)

"Tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu" (2 Wakorintho 1:9). Mtume Paulo aliandika maneno hayo wakati alipokuwa akijikwaza chini ya mwamba. Alikuwa akisema, kwa kweli, "Bwana alinileta kwenye mwisho wa usaidizi wote wa kibinadamu. Ilikuwa nimahali pasiokuwa na matumaini, ni Mungu pekee wa nguvu za ufufuo angeweza kuniokowa!"

Wakati mwingine Mungu anakuwezesha kuendeshwa hadi mwisho wa kamba yako, ndani ya mateso makubwa, ili uweze kupoteza uwaminifu yote katika uwezo wako wa kujiokoa. Ni mahali pazuri sana - mwishoni mwa kamba yako. Lakini haisikiliki vizuri sana, Je! Linatendeka? Hasa katika utamaduni ambao umekuwa umejaa kijiko ca mawazo ya kujitegemea. Tuna idadi isiohesabiwa imeandikwa juu ya jinsi ya kushughulikia shida, upweke, huzuni, majaribu. Lakini yote inazingatia mwili wetu, uwezo wetu wa kujitenga wenyewe kutoka kwa shida zetu.

Mpendwa, ni mara ngapi umejaribu kutatua matatizo yako yote na wewe mwenyewe? Labda umejaa mafuriko ambayo yalikujeruhi hadi kufikia mwisho wa kulia, "Oh, Mungu, unajua ninakupenda kwa moyo wangu wote lakini ninajaribiwa sana. Ninadharau hili, Bwana. Ivi sielewi!"

Nimejifunza somo la thamani kupitia majaribio yangu yote: Nilipata njia ya kukimbilia! "Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawacha mjaribiwe kupita mwezavyo, lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili" (1 Wakorintho 10:13).

Hii ni njia gani ya ukimbilio? Inakuja kwenye mwisho wa nguvu zako mwenyewe na kugeukia kabisa kwa Mungu. Na kusema, "Siwezi kujiamini tena mwenyewe. Mungu, ninaweka kila kitu juu yako na ninakuamini kabisa. Najua utamaliza mateso yangu kwa wakati wako na kwa njia yako!"