MWENZI WA KILA WAKATI WOTE

David Wilkerson (1931-2011)

"Wakati Yeye, atapokuja huyo Roho wa ukweli, atawaongoza kwenye ukweli wote; kwa maana hatanena kwa ajili ya mamlaka Yake, lakini chochote atakachosikia atakinena; naye atawambia mambo yatakayokuja. Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atachukua kilicho ndani yangu na kukitangaza” (Yohana 16:13-14).

Tabia ya kipekee ya Roho Mtakatifu ni kwamba hapendi kuzungumza kwa ajili yake mwenyewe. Yeye hataki tujue mengi Zaidi kuriko kujuwa kazi yake mwenyewe, ambao ni kutuleta kwa Yesu na kutufanya tuwe safi na utakatifu. Yeye yuko kazini kila wakati, kwa kufanya Kristo ajulikane ndani ya mioyoni mwetu, na anatowa furaha nyingi kutafuta kwetu kwajili ya kufahamu kwa nini alikuja.

Yesu alikuwa amekusanya wanafunzi wake kwa wakati mmoja wa mwisho wa ushirika kabla ya kutafsiri. Ilikuwa wakati wa huzuni kwao kwa sababu chanzo chao cha faraja kilikuwa kinataka kuwodolewa. Yesu alikuwa mwongozo wao na mwalimu wao, furaha yao, amani, tumaini na upendo, lakini sasa alikuwa akiwaacha kimwili. Hawakuelewa kweli zawadi iliyokuja baada ya kuagana.

Je! Unaweza kufikiria maswali waliyokuwa nayo? "Sasa ni nani atatuongoza? Tutakwenda wapi kwa maneno ya uzima wa milele? Alituambia tuende ulimwenguni kote na kuhubiri injili kwa jina lake, lakini nguvu hiyo itatoka wapi? Yeye ni yote ambao tumewahi kujua na tumejenga ulimwengu wetu wote karibu naye!” Yesu alisoma akili zao. Alijua kile kingewakabili: magumu, marudio, mateso, na hata kuteswa, kwa jina lake. "Nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi milele" (Yohana 14:16). Kisha akawahakikishia, "Sitawaacha kama yatima; Nitakuja kwenu” (ona 14:18).

Inaonekana ni rahisi kuamini kuwa Roho Mtakatifu ametumwa kwa ulimwengu, lakini ni vigumu zaidi kuamini kuwa ametumwa kwetu kibinafsi. Ikiwa Yesu angeonekana ghafla kando yako, je! Ungeongea naye? Kwa kweli ungefanya! Vivyo hivyo, Roho Mtakatifu anapaswa kuwa binafsi kwako - faraja yako, mwongozo wako, mwenzi wako wa siku zote!