MUNGU HAJAWAHI KUSHINDISHA WATU WAKE

Carter Conlon

Kwa mujibu wa kitabu cha Waebrania, kila mmoja wetu anapaswa "Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu" (Waebrania 10:32). Kumbuka jinsi Mungu mwaminifu amekuwa - jinsi alivyokulete kupitia mapigano na majaribio yako yote ya zamani. Wakati ulipofika kwa Kristo kwanza, labda familia yako yote ilidhani wewe ni wazimu; marafiki wako wa zamani hawakutaka kuwa na wewe tena. Watu wanakuhukumu mahali pa kazi kwa sababu tu ulichagua kufanya yaliyo sawa. Na sasa, tena, unakabiliwa na mashtaka mabaya kutoka pande zote. Ndio maana ni muhimu kukumbuka jinsi Mungu alivyojitokeza mwenyewe na kukuleta katika siku za nyuma. Yeye hakukushindisha, Je! Alifanya hivyo?  Je! Halafu atakushindisha katika siku zijazo.

Mwandishi wa Waebrania anasema, "Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo, tena mkakubali kwa furaha kunyang’anywa mali zenu" (Waebrania 10:34). Wengi wa waumini hawa walikuwa bado hawajateseka, lakini walikuwa wanafahamu kuwa wengine waliokuwa kwamba walio watangilia mbele yao waliteseka. Wakati inasemekana kwamba "walikubali uharibifu wa mali zao," ina maanisha kwamba walikuwa wameweka chini mipango na ndoto zao - mawazo yao yote kuhusu jinsi maisha yao yanapaswa kufanya kazi. Badala yake, walikuwa tayari kukubali mpango wa Mungu kwa maisha yao, kwa kujua kwamba ingewezekana kuwa kipimo cha mateso.

Mstari unaendelea kusema, "Mkijua kwamba muna mali bora na ya kudumu huko mbinguni" (10:34). Hii ni njia nyingine ya kujiandaa kwa wakati wa mateso. Haijalishi tunachopaswa kupitia, mwishoni kitakuwa kitu cha thamani. Kumbuka, tunapigania kitu cha milele - si tu kwa wenyewe, bali kwa wengine. Tunapigana ili tuwe na kitu cha kuachia kizazi kinachokuja baada yetu.

Carter Conlon alijiunga na jopo la wachungaji wa Times Square Church mwaka wa 1994 kwa mwaliko wa mchungaji muanzilishi, David Wilkerson, na alichaguliwa kuwa Mchungaji Mkuu mwaka 2001.