MOYO WA MCHUNGAJI

Gary Wilkerson

Maisha yangu mengi nilikuwa na dhana iliyopotoka sana ya wachungaji. Wakati niliposikia hadithi za Biblia kuhusu Daudi mchungaji, nilimchola akiketi juu ya mwamba, akicheza ngoma yake na kuangalia kondoo wakati wakimzunguka wakiwa kimya. Lakini nilikuwa na picha tofauti kabisa ya wachungaji nilipowaona kwa wenyewe huko Romania miaka michache iliyopita. Wanaume wanaofanya kazi kwa bidii walikuwa wakitafuta daima maeneo yenye kuwa na majani safi ya kulisha na maji ya kunywesha. Waliamka asubuhi na mapema, wakiongoza kondoo na kutaka mahitaji yao, na kurudi baada ya siku kamili ya kutembea, kwa kawaida wanafanya kazi angalau saa kumi na nne kwa siku nyingi.

Daudi ni mfano mkamilifu wa shujaa wa mchungaji - anayeweza kupigana, kuimarisha na kuimba wakati huo huo. Moyo wa mchungaji hauna ubinafsi, tayari kutoa maisha yake mwenyewe kwa ajili ya kondoo wake. Pia, moyo wa mchungaji ni kinga na dhabihu. Mara nyingi adui hutishia kondoo, na mchungaji ni lazima awe macho wakati wote. Daudi alimwambia Mfalme Sauli wakati aliposubiri kupigana na Goliathi mkuu: "Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na wakati simba au dubu ilikuja na kumchukua mwana-kondoo katika kundi, mimi hutoka nikamfuata na kulipiga, na kumtoa mwana-kondoo kutoka kinywa chake" (1 Samweli 17:34-35).

Hakika huu sio mchungaji ambaye alikuwa akipumzika kwa muda kwa kulala katika jua la maghaibi, akipiga gita yake na kukishika kwa rahisi. Hapana, alikuwa na macho yenye kuwa tayari kufanya vita. Na Daudi alikuwa shujaa wa kushangaza. Alikuwa anatoka kwenye ushindi na kuingia kwenye shindi akiwa na moyo wa kuimba.

Mungu hakutufanya sisi tu kuwa mashujaa, yeye pia hutufanya sisi kuwa waabudu. Anatufanya sisi kuimba bila kujali yenye adui atatutupia. Daudi alikuwa na wimbo wakati simba walifika kwake na wakati dubu alimtishia kwa sababu alijua jinsi ya kujihimiza mwenyewe ndani ya Bwana. Aliimba hivi: "Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa ... Hunirudishiaa nafsi yangu" (Zaburi 23:1-3).