"MIMI SINA OMBI ILA KRISTO TU"

David Wilkerson (1931-2011)

Kila mwaminifu katika Kanisa la Yesu Kristo anaitwa kuwa mtakatifu - safi na asiye na hatia machoni pa Mungu. Kwa hivyo, ikiwa umezaliwa tena, utakatifu lazima uwe kilio cha moyo wako. "Mungu, nataka kuwa kama Yesu. Nataka kutembea mbele katika utakatifu siku zote za maisha yangu."

Agano Jipya linatuambia kama tumeitwa kuwa watakatifu "kama Mungu alivyo akiwa mtakatifu." Je! Duniani tunafanywa utakatifu machoni pa Mungu?

"Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi kueni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, mtakuwa 'Watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu'" (1 Petro 1:15-16).

Unaposoma Agano Jipya juu ya suala hili, unaweza kulalamika. "Unamaanisha kwamba mimi ni  mtakatifu kama Yesu alivyokuwa? Haiwezekani! Alikuwa hana doa, mkamilifu. Ni jinsi gani katika dunia kunaweza kuishi mtu furani kwa kiwango hicho? "

Hiyo ndio madhumuni ya sheria - kutuonyesha kwamba haiwezekani kwa mtu yeyote kupima kiwango cha Mungu cha utakatifu. Kwa hiyo, ikiwa hakuna mtakatifu lakini Bwana tu, kuna njia moja tu ya kuwa mtakatifu. Lazima tuwe ndani ya Kristo na utakatifu wake lazima uwe utakatifu wetu.

Paulo anasema kwamba kwa sababu Yesu, mzizi, ni mtakatifu, basi sisi, matawi pia nitakatifu (tazama Warumi 11:16). Na Yohana anaandika, "Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi" (Yohana 15:5). Kwa maneno mengine, kwa sababu sisi ni ndani ya Kristo, tunatakaswa kwa sababu ya utakatifu wake.

Yesu anasimama peke yake katika utakatifu mkamilifu na kama mtu yeyote anaweza kusimama mbele ya baba wa mbinguni na kupokea na yeye, mtu huyo lazima awe ndani ya Kristo. Sala yetu ya kila siku inapaswa kuwa: "Bwana, mimi sina ombi ila Kristo tu. Ninakuja kwenu tu kwa sababu mimi niko ndani ya Kristo na ninasema utakatifu wake. Najua mimi nimesimama mbele yako bila kufungwa kwa sababu mimi ni ndani yake!"