MAOMBI ANAOJIBU ZAIDI

David Wilkerson (1931-2011)

Wakati mwingine Mfalme Daudi alimwomba Mungu amokoe kutoka kufa, na Mungu akajibu sala yake: "Alikuomba uhai, ukampa - mda mrefu wa siku nyingi" (Zaburi 21:4). Lakini Mungu aliendelea zaidi katika kujibu sala ya Daudi. Sio tu alimpa uzima, naye pia akaweka taji juu ya kichwa chake na kumfanya awe mfalme wa Israeli.

Baada ya Mungu kumfanya Daudi mfalme, akamumwangia heshima na utukufu juu yake. "Umemvika taji ya dhahabu safi kichwa chake. . . Heshima na adhama waweka juu yake" (2:3 na 5). Na juu yake, Mungu aliongeza furaha kubwa: "Wamufurahisha kwa furaha ya uso wako" (21:6).

"Maana kwa Bwana kuna . . . kuna ukombozi mwingi" (Zaburi 130:7). Daudi alikuwa akisema, "Bwana, hamkunitia huruma kwangu lakini umemwaga ukombozi wako."

Mwana wa Daudi Sulemani pia aliomba sala rahisi: "Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?" (1Wafalme 3:9). Sulemani alikuwa akisema, "Bwana, yote ninayotaka ni hekima ya kujua jinsi ya kushughulikia watu wako. Mimi nataka tu kuwa mfalme wa haki juu yao."

Mungu alijibu ombi la Solomoni moja kwa moja kwa njia ya ajabu: "Mungu akamwambia, kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala haukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu, basi, tazama, nimefanya kama ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu kama wewe, wala baada yako hatainuka mtu kama wewe" (3:11-12).

Mungu alifurahia sana kujibu zaidi maombi ya kutokujipenda kwa matu wakubwa hawa! Na Baba yenu wa mbinguni anataka kufanya vivyo hivyo kwa ajili yenu.