KWENDA MBALI UKIWA PAMOJA NAYE

David Wilkerson (1931-2011)

Ufunuo mkubwa zaidi ambao wanafunzi walikuwa hajawahi kuupata ulikuwa unazingatia ufufuo wa Yesu Kristo. Ilikuwa siku ya kwanza ya juma, na wanafunzi walikuwa wamejificha nyuma ya milango imefungwa kwa ajili ya kuogopa Wayahudi. Ghafla, Yesu alionekana - katika utukufu kamili wa ufufuo - kushinda kifo, kuzimu, na shetani. Aliwaonyesha wanafunzi mikono yake, miguu yake, upande wake uliovunjwa, halafu akawajaza na kusema, "Pokea Roho Mtakatifu" (Yohana 20:22).

Utukufu gani wa kweli uliokuja - ufunuo juu ya ufunuo! Ilikuwa karibu kuwazidia sana wanafunzi, na wengi wao, wakiongozwa na Petro, waliamua kwenda kuvua (tazama Yohana 21:3). Petro alikuwa na shida akichukua yote ndani. "Siwezi kuelewa msalaba – Je! Ni aje nitaweza kuelewa ufufuo wake? Baada ya wakati huu wote nimetumia pamoja naye, nimeelewa kidogo sana. Hebu acha wale ambao ni shujaa waende pamoja naye. Ninataka tu kufanya jambo langu mwenyewe, kwa njia yangu ya utulivu."

Wengi wetu tunaweza kuitikia mambo ya kiroho kwa njia ile ile. Tunajua Bwana ametuita kutembea zaidi pamoja naye, lakini tunaepuka changamoto. Tunarudi kwenye njia zetu za zamani na kisha tunajisikia kuwa wenye hatia kwa uthabiti wetu. Tunaogopa kama hatuwezi kamwe kupima kile ambacho Mungu anataka kwetu ili tupate kurudi kwa kwa shuguli zetu- ununuzi wa vitu, vituo vya kujifurahisha, miradi mipya. Wakati mmoja uliotumiwa pamoja na Mungu katika kukua hupotea kwa namna fulani ya "uvuvi" na tunakuwa wafuasi na wasio na uhakika.

Wakati Petro alikuwa kwenye kivuvi, Bwana aliona kwamba hawakuwa na kitu chochote na akamwongoza kutupa nyavu yake upande wa pili - ambapo alikusanya mavuno makubwa ya samaki. Baadaye, wakati Petro alipokuwa anachaguwa samaki zake, Yesu akamwambia, kwa kweli, "Petro, ikiwa unanipenda, rudi mahali ulipokuwa. Nifuate; ili kulisha kondoo wangu; acha kufanya jambo lako mwenyewe. Amka!" (Angalia Yohana 21:15-18).

Yote amabayo Yesu anakuuliza ni kwamba unampenda. Usijali kuhusu kupimwa na usiruhusu ukame wako kuludilia ili ukuleteye kukata tamaa. Furahia ndani ya hao - ni sehemu ya mpango wa Mungu wa kukuletea kusudi lake kwa maisha