KUTOKA KWENYE BANGO LA MAOMBI HADI KWENYE SHIMO LA SIMBA

David Wilkerson (1931-2011)

Biblia inaonyesha mfano katika maisha ya watu wote wa Mungu. Katika kesi baada ya kesi, wakati Mungu alianza kutekeleza ahadi zake, dari ilikuwa inaonekana kutumbukia ndani.

Fikiria Danieli, kijana mzuri, mwenye vipawa ambaye alichaguliwa kutumikia katika nyumba ya mfalme (angalia Danieli 1:3-6). Aliahidi mwenyewe kuishi maisha ya utakatifu na kujitenga na ulimwengu, na kukuzwa kwa sababu ya ubora wake. "Basi Danieli huyo alipata sifa kuliko wakubwa  .... Kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaamru kumweka juu ya ufalme wote" (Danieli 6:3). Lakini watu wenye ulaghai wakawa na wivu, na wakafanya njama za kumwangamiza Danieli, na kusababisha kutupwa kwake katika shimo la simba. Mungu aliingilia kati na akamwokoa mtumishi wake kwa kufunga midomo ya simba!

Fikiria Shadraki, Meshaki na Abednego, vijana watatu wa kipekee walioletwa kwenye nyumba ya mfalme, ambapo walifanywa kuwa viongozi katika serikali. Hata hivyo, wakati mfalme aliamuru kila mtu ainame mbele ya mungu wake wa uongo, walikataa na mara moja wakafungwa na kutupwa katika tanuru la moto iliyoandaliwa kwao. Wote walionekana kuwa wamepotea mpaka Mwana wa Mungu alipojitokeza katikati ya moto na kuwaokoa!

Na fikiria Eliya. Mungu alimpa ahadi ya utukufu wa uamsho wa kiroho katika nchi, wa umwangiliaji wa mvua nyingi, na siku mpya ya ushindi kwa watu wa Mungu. Ahabu mbaya na Yezebeli walipaswa kupinduliwa ili amani itawale ufalme wote. Lakini Yezebeli alitishia maisha ya Eliya, manabii wa Mungu waliuawa, na nchi ikaendelea katika uovu na ukame. Eliya alijihisi peke yake na kuchanganyikiwa kabla ya ahadi hiyo. Soma kifungo hiki katika 1 Wafalme 18 na 19.

Usizuiliwe na hali mbaya, hali ya kuchanganyikiwa katika maisha yako. Moja haitoke kwenye bango la maombi kwenda kwenye ushindi wa mlima. Unaweza kwenda kwenye shimo la simba, au tanuru la moto, au bonde la machafuko. Lakini usivunjike moyo! Mungu ni Mwenye nguvu na Mchungaji, na bado anaendelea kuongoza. Mateso yako na machafuko atatoa njia ya imani ambayo haishindwi kamwe - imani ambayo imejaribiwa, kama dhahabu, katika moto wa mambo mbali mbali.