KUTEMBEA KATIKA AHADI ZA MUNGU

Gary Wilkerson

Wakati Yoshua alipopewa ma muraka ya kuwa kiongozi wa taifa la Waisraeli, Mungu alisema kwa maneno mazito kuhusu yeye . "Je! Si mimi niriye kuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendapo" (Yoshua 1:9).

Mungu alikuwa akimwambia Yoshua, "Uwe na moyo na usiogope. Kuwa na nguvu kwa kuwa ninawaongoza katika kitu kikubwa." Sasa Yoshua alikuwa tayari kuchukua uongozi katika mpango mkuu wa Mungu, mambo  angeenda kutokea ambayo hayajawahi kutokea hapo awali. Lakini Yoshua alikuwa tayali kwa kusimama na kuingia katika ahadi za Mungu.

Yoshua alikuwa akifanya kazi pamoja na Musa, akipigana vita vingi na kushinda,  kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye. Alikuwa mwaminifu na mtiifu kwa wito wa Mungu na imani yake yenye kukomaa imemfanya awe kiongozi mkubwa.

Musa alipokufa, Mungu akasema, "Yoshua, ni wakati!" Ni jambo lenye kusisimua sana kusikia Mungu akisema kuwa ni wakati. Yoshua alikuwa akingojea,  na baada ya miaka arobaini ya kutembea kwa njia ya jangwani, alikuwa na furaha, fursa, nafasi ya kuwaambia watu wake, "Tunavuka!"

Fikiria mwenyewe ukienda katika Nchi ya Ahadi pamoja na watoto wa Israeli. Furaha hiyo! Kucheza na kuimba mbele za Bwana, "Tuliifanya - hatimaye. Tuko hapa! Halleluya! Baada ya miaka yote ya kusubiri na kutembea, sisi hatimaye tunapata ahadi."

Je, umesubiri kutimiza ahadi ya Mungu? Vita yako haijawa nje, bali pia katika moyo wako. Ninakuhimiza kuamini kwamba vitu vingi vinakuja kwako. Mungu ataingilia kati katika mazingira yako na utaenda katika vitendo vyako.

Faraja moja ambayo Mungu alimpa Yoshua inaweza kutumika kwako, pia. "Uwe na nguvu na ujasiri. Bwana Mungu wako yu pamoja nawe popote unapoenda. "Kama wewe ni mwaminifu kwa Mungu, atakuwa mwaminifu kwako.