KUSHIKWA NA MAOMBI YA KRISTO

David Wilkerson (1931-2011)

"Bwana akasema, Simoni, Simoni! Tazama, Shetani amewataka ninyi, ili apate kuwapepeta kama vile ngano. Lakini nimekuombea wewe, ili imani yako isije isitindike” (Luka 22:31-32).

Yesu alikuwa ameshuhudia uporaji ambao ulikuwa unamkujia Petro, na hakuuziwiya kwa sababu mchakato ulikuwa ni lazima. Lakini Yesu akaongeza haraka, "Nimekuombea." "Nimekuombea" sio "nitakuombea." Labda alikuwa amekaa masaa mengi na Baba akizungumza juu ya Petro - jinsi alivyompenda, jinsi alivyokuwa akihitaji kuwa katika ufalme wa Mungu, jinsi alivyomthamini kama rafiki. Wakati Yesu alisema alikuwa akimuombea, alikuwa akizungumza sio tu na Petro, bali na wanafunzi wote - na sisi leo.

Yesu alijua vizuri kabisa ukali wa nguvu za uovu na jinsi Shetani anavyopiga wafuasi wa Bwana. Hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuelewa ugomvi mkubwa unaoendelea hivi sasa katika eneo la roho dhidi ya watakatifu ambao wameweka mioyo yao kwa dhati kuendelea na Kristo.

Katika kutembeya kwako kwa Kikristo, inakuja wakati ambao unavuka mstari wa kuingia katika maisha ya utii na utegemezi kwa Yesu, umeamua moyoni mwako kamwe usirudi nyuma. Wakati hii inafanyika, unakuwa tishio kwa ufalme wa giza, na kwa hivyo, kuwa shabaha ya wakuu na nguvu. Ushuhuda wa kila mwamini anayemgeukia Bwana kwa moyo wake wote, njaa ya utakatifu na kutembea sana na Yesu, ni pamoja na kuzuka kwa ghafla kwa majaribu makali!

"Yesu ... akainua macho yake mbinguni, akasema ..." Ninawaombea ... Baba Mtakatifu, uwalinde kwa jina lako wale ambao umenipa ... siombe kwamba uwawondoe ulimwenguni, lakini kwamba Wewe uwalinde yule mwovu ” (Yohana 17:9, 11, 15).

Ikiwa umejitowa kabisa kwa Mungu - kusoma Neno lake, kutumia wakati pamoja naye, kupenda roho zilizopotea - haijalishi unapitia nini au ni nini mbele yako, Yesu anakuombea. Faraja gani nzuri kwa kila mtoto wa Mungu!

Tags