KUPITIA KILA JARIBIO

David Wilkerson (1931-2011)

Tunafanya uchaguzi ya kuishi maisha yetu yenye kujaa hofu kilamala au yenye kuamini mu Mungu. Ikiwa leo tunaruhusu sisi wenyewe kuwa na wasiwasi juu ya jambo moja, tutakuwa na wasiwasi kuhusu mambo mawili ya kesho. Kwa kifupi, hofu zetu zitaendelea kuongezeka kuwa mulima, kama mawimbi ya matatizo yataendelea kuja. Na kisha, ikiwa hofu zetu hazikaguliwe, akili yetu yakuwa nawasiwasi itaendelea kushuka kwenye shimo la chini.

Tunapaswa tu kuwa na hakika kwamba tunapendwa na Baba yetu wa mbinguni, hayijali jinsi majaribio yetu ni makubwa. Tunaweza kusikia sauti za hofu zikicheza kati ya mawimbi ya kuongezeka kwa shida, lakini Daudi alishuhudia kiuwazi: "sauti ya Mungu inasikika juu ya mafuriko!" "Bwana aliketi juu ya Gharika, naam, hali ya mfalme milele" (Zaburi 29:10).

Wakati mafuriko makubwa anakuja katika maisha, watu hupata "giza la ghafla la imani." Ushuhuda nilisha wahi kusikia wote unakitutaniya kwenye kitu kimoja: nafusi yenye usiku wa giza. Nimethibitishiwa miaka mingi ambayo kila mtumishi mwaminifu wa Kristo anakabiliyana na mgogoro huo mala yakwanza au mala nyingine. Nimezungumza na wale ambao walielezea wakati ambapo kila kitu kilionekana kiko chini ya wingu la giza, na sauti ya Mungu ilikuwa kimya. Walifanya kila kitu walichojua ili kujaribu kusikia sauti kutoka mbinguni, lakini giza liliendelea tu.

Ni wakati tu vile Maandiko yanasema tunapaswa kujua na kuamini upendo Mungu anao ajili yetu. Wakati dunia yetu inapopindukia chini, tunakuwa kwenye hatari yakukabiliwa na uongo wa adui. Shetani atajaribu kutumia matatizo yetu ili atulete shimoni la kukata tamaa. Katika nyakati hizo ni muhimu kwamba tuchukue ujuzi wetu kuhusu upendo wa Mungu ajili yetu.

Katika maisha yangu, nilikuwa na majaribio mengi yaliomwagiwa kwangu. Na hii ni moja la ukweli ambayo imeniunganisha kwa yote: Mungu ananipenda wakati wote, kupitia kila jaribio la maisha.