KUPATA TUZO

Gary Wilkerson

Katika utamaduni wa leo, Wakristo wengi wanachanganyikiwa juu ya dhana za kushinda. Lakini mara nyingi inaonekana kama hatujui jinsi ya kufafanua manayake kushinda . Wachungaji wanafikiri kwamba ili wawe na kanisa la kushinda wanapaswa kuwa na jengo kubwa, bajeti iliyoongezeka, timu ya ibada yenye ufanisi, na kuwa na huduma ya watoto bora. Wafanya biashara wanafikiri kwamba kuwa na wafanyakazi zaidi, kufurahia faida kubwa, na kufikia ufahari katika uwanja wao wakushinda pesa nyingi. Mambo haya yote ni mazuri, bila shaka, na kwa maana moja, ni kushinda. Lakini Paulo anafafanua kushinda njia nyingine na hutuletea msingi wa ujumbe wa Mungu, Injili ya Yesu Kristo, na jinsi ya kupata tuzo.

"Ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie tuzo la mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu" (Wafilipi 3:13-14).

"Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate" (1 Wakorintho 9:24). Paulo anaendelea kusema kwamba yeye si "kupiga hewa" kwa uwazi, akiwa na kutokuwa na uhakika (9:26). Yeye anajipatiya adabu ili asishindwe katika mbio. Wakristo wengi leo wanazunguka katika mielekeo kadhaa tena tofauti, wakitafuta juhudi mbalimbali za huduma na njia za kujitegemea. Kwa kweli, wanaweza kuwa wanafanya mambo mema mengi, lakini kwa kweli hayatimizi kushinda ambao Paulo anazungumzia - kupata watu kwa kupitia mstari wa mwisho.

Hebu tuchague kuwa kama Paulo. Wote wanaotuzunguka sisi ni wale watu wamevunjika moyo, bila Yesu, wamefungwa na dhambi na kwanda  mbela mile na milele bila Mungu. Lazima tuwaambie habari njema ya Yesu Kristo - kwamba alikufa msalabani kwa ajili yao  ili waweze kuwa safi na watakatifu. Ushindi mwingine! Tuzo lingine!