KUOMBA KABLA YA MGOGORO

David Wilkerson (1931-2011)

Wakati Yesu alipokuwa akitembea hapa duniani, alijihusisha na watu wote. Alifundisha katika masinagogi, juu ya milima na kwenye boti, akiponya wagonjwa na kufanya miujiza. Aliinua sauti yake kwenye sikukuu, akalia, "Mimi ni maji yaliyo hai! Njoo kwangu na nitamariza kiu ch nafsi yako." Mtu yeyote anayeweza kumkaribia na ataridhika. Lakini mwaliko wa Bwana wetu ulipuuzwa zaidi.

Yesu alilia juu ya watu, "Ewe Yerusalemu, Yerusalem, uwauaye manabii, nakuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Nimara nagapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!" (Mathayo 23:37). Alikuwa akiwaambia Waisraeli, "Mimi niko hapa sasa, napatikana. Nimekuambia uje kwangu kwa uponyaji na kuwa na kuona kwamba mahitaji yako amefikiwa, lakini haukuweza kuja."

Yesu akajibu kwa watu waliomkataa kwa kutangaza, "Angalieni! Nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa" (23:38). Neno ambalo Yesu anatumia kwa ukiwa hapa linamaanisha upweke, kutokuwa na matunda, taka. Anasema, "Maisha yako ya kanisa, familia yako, kutembea kwako kwa kiroho yote yanakwenda kukauka na kufa."

Baba wetu wa mbinguni anajali sana kuhusu shida za watoto wake wote. Wakati wowote tunakabiliwa na nyakati ngumu, anatuhimiza tukaribie, akisema, "Njoo, uinue mateso yako yote, mahitaji na malalamiko mbele yangu na nitasikia kilio chako na kujibu." Anatamani sisi tuone kiu baada yake, kama vile mtunga-zaburi alivyosema: "Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu" (Zaburi 42:1-2).

Usisubiri mpaka mgogoro unatokea ili umkaribie Mungu. Anatamani sana wewe umupatie yeye roho yako yote kwa upendo na kuabudu kwa msingi wa daima.