KULEMEWA NA MZIGO ZAIDI YA KIPIMO

David Wilkerson (1931-2011)

"[Mungu] aliyetuokowa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; amabaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa" (2 Wakorintho 1:10).

Paulo anasema hapa juu ya nguvu za Mungu za kutoa - zamani, sasa na baadaye! Anasema, "Mungu ametuokoa katika siku za nyuma, yeye anatuokoa sasa, na atatuokoa katika shida na majaribio yote ya baadaye. Hatuezi kuwa naoga wakila kitu chochote kinachokuja kwa njia yetu kwa sababu tunamjua Mungu atatuokoa!"

Hilo ni tamko lenye nguvu lakini wengi wetu tunasahau uokoaji uliopita wa Bwana wetu, kama vile watoto wa Israeli walivyofanya. O, Mungu aliwapa wukombozi! Kuwaongoza kwa wingu mchana na moto usiku; kugawanya Bahari ya Shamu ili waweze kuvuka kwenye nchi kavu; kuwapa mana kutoka mbinguni na mito ya maji nje ya mwamba. (Soma hizi katika Kutoka 13:21, 14:21-22; 16:31; Zaburi 78:16.) Lakini bado waliendelea kumjaribu Mungu na kumwambia maneno ya kumupinga.

Kwa kusikitisha, mara nyingi hutokea kwetu pia. Tunasema, "Naam, nilikuwa nimefungwa sana imara, na Mungu aliniokoa. Lakini hii ni tofauti."

Baba yetu mwenye upendo anataka tupate mahali pa imani yetu ambapo tunamwamini katika kila mgogoro, kila jaribu, bila swali. Anataka sisi tusiwe nashaka kuhusu nguvu zake za kutuokoa.

Usielezee mimi. Bado tunapaswa kupigana vita vizuri vya imani. Bwana ana njia ya kuturuhusu "kuwa na mzigo zaidi" wakati mwingine, kama Paulo anavyoandika katika 2 Wakorintho 1:8. Hii ina maana kwamba alijaribiwa zaidi ya nguvu zake mwenyewe na hakuweza tena kujiamini. Kwa hivyo akageukia Mungu!

Wakati mwingine tunapaswa kukubali kwamba tuko juu ya kichwa chetu na kutia magoti mbele ya Bwana! Ninakuhimiza kulilia Bwana leo na kumwamini. Yeye ni mwaminifu wa kukuokoa.