KUKABILIYANA NA ADUI KWA UJASIRI

Nicky Cruz

Ikiwa tunaliamini au la, ni kweli kwamba Shetani yuko kwenye ujumbe - ujumbe ulivyo rahisi kama kwa nia moja. Yeye yuko nje ili aibe nia yetu na ameamua kuitimiza. Fikiria jinsi anaweza kuwa na ufanisi kama anaweza kutekeleza kazi hii moja - hii moja ya kutafuta. Kitu hiki anachohitaji sana kufikia.

Ikiwa Shetani anaweza kuiba nia yetu, tuondoe msisimko wetu kwa ajili ya Yesu, tuendelee kuzingatia mawazo ya kushinda roho za watu na kufikia ulimwengu kwa ajili ya Kristo, anaweza kushikilia uzibiti wa kikamilifu hapa duniani. Anajua ukweli huo, na anafanya kazi kwa kila kitu chenye uhai wake ili kuona kinatokea. Ni mbali kwa njia nyingi sana anafanikiwa.

Mara nyingi Wakristo hukasirika na kulalamika kuhusu siku zijazo; wanalia na kuomboleza kuhusu ushindi mwingi wa Shetani ulimwenguni, jinsi anavyoshinda vita nyingi na kupata vuguvugu la kundi kubwa nchini humu, hata duniani kote. Wanasema kama Shetani anaelekea kushinda. "Tunapoteza watoto wetu kwa ajili ya utamaduni," wanasema. "Makanisa yetu yanakufa kwa idadi kubwa, na jamii yetu inaongezeka zaidi ndani ya uovu siku hizi." Mimi naliona mwenyewe, lakini najua kwamba wakati Shetani akishinda, ni kwa sababu watu wa Mungu wanaoga badala ya kusimama, na wanakabiliane na adui kwa ujasiri. Wao wanajiondowa kwa urahisi sana. Neno la Mungu linatuambia, "Wakati adui atakuja kama mafuriko, Roho wa Bwana atainuka ili akabiliyane naye" (Isaya 59:19).

Ninatamani kuona siku ambapo Wakristo wanasimama bega kwa bega, mkono kwa mkono, katika vita hivi na Shetani na hatimaye kuchola mstari katika mchanga, mwembamba wa njia yake. Unaweza kuwa sehemu ya jeshi hili la askari lililoinuka dhidi ya Shetani katika siku hii. Hebu acha moyo wako uashwe na Roho Mtakatifu, na uwe shujaa katika vita hivi vikubwa kwa ajili ya Mungu. Vita viko vinalipwa, kwa hivyo chukua upanga wako na kupate nafasi yako ndani ya safu yake!

Nicky Cruz, mwinjilisti wa kimataifa aliyejulikana na mwandishi mkubwa, alimgeukia Yesu Kristo kutoka kwenye maisha ya vurugu na uhalifu baada ya kukutana na David Wilkerson huko New York City mwaka 1958. Hadithi yenye kushangaza  ya kuokoka kwake ilisemwa mara ya kwanza katika Musaraba na Kisu kinachomoka ( Cross and Switchblade) na David Wilkerson na kisha baadaye katika kitabu chake chenye kuuzwa vizuri zaidi, kiitwaco:Kimbiya , Mtoto, Kimbiya (Run, Baby, Run).