KUJIANDAA KWA AJILI YA VITA

Gary Wilkerson

"Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kupitana hila za shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya ufalme na mamlaka, juu yawa kuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho ... Kwa sala zote na maombi mkiomba kila wakati katika Roho" (Waefeso 6:10-12, 18).

Katika sura tano za kwanza za barua yake kwa kanisa la Efeso, Paulo aligundua vitu vya ajabu ambavyo Roho Mtakatifu alikuwa amekamilisha na alifurahiya ukuaji wa kiroho ambao ulifanyika maishani mwao. Katika sura hii ya kumalizia, anawapa neno la tahadhari kwao juu ya upinzani unaowakujia - na mahitaji yao ilikuwa kujiandaa.

Akiongozwa na Roho Mtakatifu, Paulo aliwafundisha Waefeso kwa uangalifu katika vita vya kiroho. Kwanza, aliwaonya kwamba nguvu za giza zitakuja juu ya dhidi yao ili kuwaibia urithi wao - na alirudilia neno juu mara kadhaa. Haikuwa kama adui angekuja juu yao, lakini ni lini na mara nyingi na ningumu kiasi gani. Kwa hivyo, aliwaambia kuwa na nguvu katika Bwana na kumtegemea, kwa sababu kujaribu kupigana kwa nguvu za mtu mwenyewe haitoshi.

Kwenye Waefeso 6:14-17, Paulo anafafanua silaha zote za Mungu ambazo zingewaandaa kikamilifu:

  • Ukanda wa ukweli
  • Kinga la kifuani la haki
  • Viatu vya Mungu kwa miguu yako
  • Ngao ya Imani
  •  Kofia ya wokovu
  • Upanga wa Roho

Unahitaji kuelewa kuwa unapigana na nguvu za uovu za kiroho. Wewe ni raia wa mbinguni, Mkristo anayeamini ukweli, na anapigania ukweli. Kwa kuishi maisha ya mshindi, Vaa “silaha yote ya Mungu” na jitayarishe kwa ajili ya migogoro. Soma Neno la Mungu, omba kwa roho, na utaweza kusimama kama mshindi baada ya vita, ukimpa Mungu utukufu wote.