KUHARIBU KUNDI ZIMA

David Wilkerson (1931-2011)

"Basi Mungu wa Amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu, awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kufanya mapenzi yake, naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake, kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele" (Waebrania 13:20-21).

Ni furaha ya kuwa karibu na watu ambao wana kusudi la kuwa na harufu ya kuwa pamoja na Yesu na wanaishi aina hii ya maisha ya Kristo. Kama Paulo, watakatifu hawa wanatamani kuwa mbele ya Kristo. Wana njaa ya kupata urafiki zaidi na zaidi na yeye na hutoa upendo na utakatifu wake.

Watu hao hufurahia maisha lakini pia huepuka mazungumzo yote ya kipumbavu. Wao wanaishi kabisa kwa kujitenga na vitu vya ulimwengu huu, na neema ya Mungu inaonekana katika maisha yao na familia zao. Wengine wanaweza kuwa masikini katika vitu vya kimwili lakini maisha yao yanabarikiwa kabisa na Bwana.

Usifanye vibaya; Waumini hawa hupitia wakati wa majanga makubwa na majaribio lakini, kama Paulo, ingawa wanaweza kutupwa chini, hawaangamizwe. Na hawakuacha kamwe! Wao niya yao ni ya kumaliza safari yao ya imani na huduma kwa namna inayompendeza Mungu.

Lakini Shetani ameamua kuweka mambo katika maisha yako ambayo huzuia kuingia katika wingi wa baraka za Kristo. Paulo alitambua hili na akawaambia Wagalatia, "Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msitii ukweli? Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi. Chachu kidigo huchachua donge zima" (Wagalatia 5:7-9). Kwa maneno mengine, "Ni nini katika maisha yako ambacho kinakuzuia kuendelea na baraka kamili za Kristo?"

Hii ni onyo nzuri kwetu leo. Wakristo wengi ambao mara moja walitumiwa kwa nguvu sana na Mungu wameruhusu kitu kuingia katika maisha yao na wamefanya amani na maelewano hayo. Kuwa mwangalifu usiruhusu dhambi moja kuwa kama chachu kidogo ambayo inaharibu kundi zima.