KUCHUKIWA BILA SABABU

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alisema alikuja kutafuta na kuokoa waliopotea. Huyu alikuwa ule Mmoja aliye na uwezo wa kushinda upepo na mawimbi, lakini alikuja kama mtumishi mnyenyekevu. Injili zinatuambia kwamba alisikiliza watu kwa uvumilivu kilio chao. Watu wengi walimsihi Kristo kuwaokoa kutokana na mateso yao na alikutana na mahitaji yao. Aliwaponya wagonjwa, akafungua macho ya kipofu, masikio ya viziwi yaliyozibwa, akafunguwa ndimi zenye kufungwa, na akafanya walemavu kutembea. Yesu aliwaweka huru mateka kutoka kila aina ya utumwa - hata alifufua wafu.

Hakuna aliyewahi kupenda wanadamu kuliko Yesu; alihuzunika juu ya makundi mbele yake, akiwaona kama kondoo waliopotea wanaohitaji mchungaji. Ukweli ni kwamba, hakuna mtu katika historia anapaswa kuwa na heshima zaidi, kuheshimiwa na kupendwa kuliko Yesu Kristo. Alifanya kazi za huruma kwa watu waliokutana nao; alilia juu ya upofu wa kiroho wa ulimwengu na akamwaga maisha yake kwa wote. Lakini licha ya mambo mema ambayo Yesu alifanya, ulimwengu ulimchukia bila sababu.

Je, Yesu alifanya nini kwamba anapaswa kudharauliwa sana, katika siku yake mwenyewe na leo? Kuweka tu, ulimwengu ulimchukia kwa sababu alikuja kama nuru ya kuwaokoa wote kutoka gizani. Alitangaza: "Mimi ni nuru ya ulimwengu. Yeye anifuataye hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima" (Yohana 8:12). Yesu pia alituambia, "Kila mtu atendaye mabaya huchukia nuru, wala haji kwenye nuru, ili matendo yake asije yakakemewa" (Yohana 3:20).

Yesu aliahidi kuwaokoa watu kutoka minyororo yao ya giza na kuahidi kuweka watu kwa kila mahali kuwa huru kutoka nguvu zote za shetani. Hata hivyo, kile ambacho sisi Wakristo tunaona kama karama takatifu ya ukombozi na uhuru, inatazamwa na ulimwengu kama aina ya utumwa. Watu hao hupenda dhambi zao na hawana hamu ya kuwa huru kutoka kwazambi.

Nuru ya ulimwengu imekuja na inakaa ndani yako. Unapokubali ukweli huu na kutembea kwa Roho, utaweza kuangaza nuru yake kwa wale walio karibu nawe.