KUCHUKIA DINI

Gary Wilkerson

Kwa sababu nataka watu wote ulimwenguni kujua ukweli wa Yesu, ninatumia muda mwingi wa kutembea duniani kote katika huduma. Na kisha nitakaporudi nyumbani, ninaomba kwamba kila Mkristo atamjua Yesu pia!

Natumaini umepata utani - lakini unahitaji kujua kama nina nusu tu ya kutania. Maisha yetu kama wafuasi wa Kristo sio juu ya dini inayojulikana, lakini juu ya Mtu anayeweza kujulikana, Yesu. Kuna tofauti kubwa.

Biblia inatuambia mambo matatu yanayotupinga sisi katika kutembea na Kristo: dunia, mwili wetu na shetani (tazama Waefeso 6:12). Nimejiuliza, "Kwa nini dini sio ndani ya orodha hiyo wakati inapinga uhusiano wetu na Yesu, pia?" Kisha nikaona dini ni katika yote matatu!

Wakati ninapotumia neno "dini,” nina maanisha mambo ya wudini. Hili ni wazo kwamba tunaweka dini - imani na mazoea yetu ya kitheolojia - katikati ya maisha yetu badala ya Mungu mwenye upendo. Ni ndani ya Yesu kwamba tunaishi, kupumua na kuwa na utu, sio mfumo wa imani au kazi.

Unapoiangalia kwa njia hiyo, dini inakuwa mfano wa mwili wetu, maana ya tabia yetu ya dhambi. Mwili wetu hutumia dini kama musitali wambele ili kupinga kutubu na hutufanya kujisikia vizuri kuhusu sisi wenyewe. Mjomba wangu Don Wilkerson anaita hii “kusonga mbele." Kurudi nyuma ni wakati watu wanapoanguka mbali na Yesu kwa kugeukia dhambi kubwa. Kusonga mbele ni kuanguka kwa upande mwingine, kugeuka kuelekea dini na mbali na kuwa mbali na Yesu.

Hebu aca tukumbane nalo, kwasababu dini inaweza kuwa na urahisi zaidi kuliko kujazwa na upendo wa Yesu, kwa sababu ya kuongozwa na upendo wake kunaweza kutufanya tuonekane kuwa watu wamechanganyikiwa kidogo kwa watu wa dunia.

Tafadhali usinielewe vibaya wakati ninasema tunapaswa kuchukia dini. Ninachosema ni kwamba tutachukia mambo ambayo yanaongoza kifo cha kiroho badala ya maisha ya kweli katika Kristo. Kuchukia dini haimaanishi kupenda mwili wako; inamaanisha kumpenda Yesu zaidi.