KUANGAZIA SANA KATIKA MAJARIBIO YETU

David Wilkerson (1931-2011)

"Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yoye! Mumtumikia Bwana kwa furaha" (Zaburi 100:1-2).

"Wenye haki hufurahi; Na kushangilia mbele za Mungu; Naam, hupiga kelele kwa furaha" (Zaburi 68:3).

"Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Waache wapige kelele za furaha, kwa kuwa wewe unawahifazi; Walipendalo  jina lako watafurahia" (Zaburi 5:11).

Mungu ni mwaminifu kwa kutaka watoto wake wa mtumikie kwa furaha na shauku - ambayo ni matokeo ya mmoja ya msingi wa wa kweli: sisi ni chini ya mabawa yake ya kinga! Hapendi sisi tushindwe na kushuka chini, na kuishi kama wasioamini wanavyofanya.

Biblia inakuja na hadithi za utukufu za wale ambao walichukua furaha kwa njia ya majaribio yao - hata wakati kila mtu ameacha tena. Katika mfano mmoja, Israeli wote walinung'unika na kulalamika isipokuwa watu wawili wa Mungu, Yoshua na Kalebu. Hawakuja kamwe katika imani yao na furaha, ingawa wote waliokuwa karibu nao walikuwa wamekata tamaa na kushindwa (tazama Hesabu 13).

Wengine, ni vijana watatu wa Kiebrania, Shadraki, Meshaki, na Abednego, walirukaruka kwa furaha wakisema, "Tutamtumikia Mungu wetu kwa uaminifu na furaha." Walifurahi katika Bwana, hawakutetemeka katika imani yao, kwa kuwa waliokolewa kimaajabu kutoka tanuru ya moto (angalia Danieli 3).

Mtume Paulo alisema, "Katika dhiki yangu yote nimejaa furaha yakupita kiasi" (2 Wakorintho 7:4). Uaminifu wote katika Bwana hutoa furaha. Hata leo, Bwana ana watu ambao hawawezi kuinama. Wanainua vichwa vyao kupitia majaribio yao yote na utukufu katika Bwana. Wanaangaza kama mfano mzuri wa jinsi furaha ya Bwana inavyowezekana katika majaribio yoyote.

Ikiwa moyo wako ni sawa na Mungu, una haki ya kufurahia na kutabasamu! Mara kwa mara Mungu huonyesha wazi kwamba anatamani kufurahia na watoto wake. Kumbuka, "Furaha ya Bwana ni nguvu zenu" (Nehemia 8:10).