KUAMINI MUNGU KWA AJILI YA MAITAJI YAKO

Gary Wilkerson

Wakristo wengi wanakabiliana na vizuizi vikubwa katika maisha yao: upotezaji wa kazi, ndoa yenye mafadhaiko, magonjwa, watoto wanaopambana na imani. Wanafikiria, "Siwezi kuona nyuma ya mlima huu mbele yangu. Ikiwa sina mafanikio, imekwisha!"

Haijalishi hali mbaya ya maisha yako, Mungu yuko katikati ya mambo. Yeye anapenda kuonyesha utunzaji wake na riziki kwa wale wampendao na wanamuamini. Mfano kamili wa hii hupatikana katika muujiza wa Elisha na mjane masikini ambaye alikuwa maskini na mwenye kukata tamaa. Katika nyakati hizo, wakati hauwezi kutimiza majukumu yako, wadai walichukua watoto wako na mali yako.

"Mwanamke mmoja ... alimlilia Elisha akisema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha Bwana. Na mtu aliyemkopa amekuja kuchukua watoto wangu wa kiume kuwa watumwa wake ” (2 Wafalme 4:1). Labda Elisha angempeleka hekaluni kwa ajili ya kupata msaada lakini alihisi kuelekezwa kwa mwelekeo mwingine. Alikuwa karibu kumfunua Mungu kwa vitendo maishani mwake.

Mwanamke alikuwa na mtungi moja tu wa mafuta ndani ya nyumba yake na nabii akamwagiza, "Nenda, ukope vyombo kutoka kwa jirani zako wote, vyombo - vyombo vitupu; usichukuwe vichache tu” (4:3). Kwenye maandiko, mafuta yanawakilisha baraka na rizuku ya Mungu. Elisha alimwagiza zaidi, "Kisha uingie ndani, ukajifungie mlango wewe na wanawe, kisha ukavimiminie mafuta hivyo vyombo vyote, na uweke kando vilivyo jaa” (4:4).

Mjane alitii maagizo ya nabii na alipokuwa akimimina mafuta kutoka kwenye mtungi lake mwenyewe, kilijaza mitungi iliyokopwa, moja baada ya nyingine, mpaka wote wamejaa. Kulikuwa na usambazaji wa mafuta usio na mwisho!

Wakati Mungu anatuambia ana ugavi wetu unaohitajika, sio pesa kidogo. Mungu ana kila kitu tunachohitaji - kila kitu kabisa. Mitungi katika hadithi hii inawakilisha uwezo wetu kwa imani; "mitungi" zaidi tunayomletea Mungu zaidi atatujaza. Simulizi hili linatukumbusha tumwamini kwa ugavi wetu, iwe ya nyenzo, ya kihemko, au ya kiroho.

Sio tu kwamba hitaji la mjane huyu lilifikiwa, lakini sasa alikuwa na ushuhuda wenye nguvu wa ukombozi wa ajabu kwa majirani zake. Hadithi yake inaweza kuwa hadithi yako unapoamini Mungu kwa mpango wake mwingi katika maisha yako.