KAZI YA UTULIVU YA ROHO MTAKATIFU

David Wilkerson (1931-2011)

Wakristo wengine wanakuwa kwenye shida daima na wanaonekana wakitaka kukuambia yote kuhusu matatizo wanayokabiliwa. Wanahisi haja ya kuelezea matatizo yao kwa wengine, lakini wanaonekana kusita kuyapeleka kwa Yesu, kwamba hana kitu cha kutoa.

Usielewe vibaya. Mimi siko namaanisha Wakristo ambao wanakwenda kupitia migogoro ya kweli, tena halali. Lakini ni ishara muhimu ya ukomavu sio changamoto ya Mungu kujidhihirisha kwako kwa ushahidi wazi au wenye nguvu, sauti ya ndani kabisa, Bwana anasema kondoo wake wanajua sauti yake, lakini mara nyingi sauti ambayo Mungu hutumia na watu wake leo ni Neno lake lililofunuliwa. Tunasoma hivi: "Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwasehemu nyingi na kwanjia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu" (Waebrania 1:1-2).

Wakati Roho Mtakatifu akisema na sisi, ni kutukumbusha maneno ya Yesu: "Lakini huyu Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliowaambia" (Yohana 14:26).

Wakati nilizungumza na kikundi cha wahudumu na nilikuwa naongozwa na Roho Mtakatifu kwa kuwa na wake wa wachungaji wa kiombeana. Kwa kuwa wanawake hawa walishikana mikono na kuombeana, uwepo mzuri wa Bwana ukawa juu yao na wakaanza kulia na kushirikiana. Hapo hakukuwa radi na umeme au ushahidi mwingine wa kawaida, lakini kitu kizuri, ni utulivu wa kazi ya Roho Mtakatifu ilikuwa inafanyika. Baadaye tulisikia ushuhuda kutoka kwa wanawake ambao maisha yao yamebadilishwa wakati huo wa thamani wakiwa na Bwana.

Usianguke katika mtego wa kutafuta ishara na maajabu; mtii Bwana tu, amini Neno lake, na umuachie matokeo yake!