KANUNI YA YESU

Gary Wilkerson

"Je! Siyo mafungo niliyoichguwa, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza Kamba za nira, kuwaachia huru walioonewa, na kwambwa muvunje kila nira?" (Isaya 58:6).

Mungu ataachili kitu kisicho na kawaida kupitia maombi na kufunga. Isaya 58:10 inatuambia, "Na kama unamukunjulia mtu mwnye njaa nafsi ilioteswa; ndipo nuru yako, takapo pambazuka gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri."

Mungu anatuambia kuwa kufunga kwa kweli kutabadili mtazamo wetu kutoka kwa kuish tukijitegemea wenyewe ili tuishi kwa ajili ya wengine; kutoka kwa kujishughulisha na kujitegemea ili kuishi maisha ya kuridhisha tamaa za waathirika. Wale wanaoishi ili kukidhi tamaa zao wenyewe wanajikuta kuepuka katika matendo yao, wamekasirika na hawana kupata utimilifu wa maisha wanayoyatafuta.

Kufunga kweli sio tu juu ya kujiepusha na chakula; ni wazo la kujitakasa kwa Mungu, kujitenganisha na kitu ili moyo wako uamke kwa kuwasaidia watu waliopigwa. Huenda ikawa watu ulimwenguni kote kupitia ujumbe au inaweza kuwa familia yako mwenyewe. Yesu alielezea kanuni hii ya kuishi maisha yenye kujali wengine.

"Naye Bwana atakuongoza daima, na ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, kama chemchemi ya maji, ambayo maji yake hayapungui" (58:11). Mungu anakupa nguvu zake, utukufu wake, kuwepo kwake wakati unapoanza kuishi kwa ajili ya wengine. Na Mungu ndiye anayetupa moyo uliobadilika ili kufanya mabadiliko haya kutokea - kuhama kutoka kwa kujishughulisha binafisi na kuwa na kujishulisha mambo ya Mungu na ya wengine.

Ikiwa utamruhusu Roho Mtakatifu afanye moyo wako na kukataa shaka na hofu na wasiwasi zisiofaa kwa mambo ya ulimwengu huu, atakubadilisha. Kitu cha kawaida kitatokea ndani yako ili kitu cha kawaida kitafanyika kupitia kwako.