KAMA VILE MUNGU ALIVYOKUSAMEHE

David Wilkerson (1931-2011)

Ikiwa unadai kuwa hauna maadui, ningependa kusikia jinsi ulivyoweza kufikia mbali katika maisha bila kuwa na mtu mmoja aliyekupinga. Hakika wakati fulani mtu amekuchukia au anajaribu kuharibu malengo yako au kupinga mipango yako. Na, ukweli ni kwamba, mambo haya yanafanya mtu kuwa adui yako.

Bila shaka, kila Mkristo anakabiliwa na adui mkubwa katika Shetani. Yesu anatuambia kwamba yeye ni adui ambaye hupandikiza kimbunga katika maisha yetu (tazama Mathayo 13:39). Vivyo hivyo, mtume Petro anatuonya kuhusu Shetani: "Jihadhari na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze" (1 Petro 5:8).

Yesu anaweka wazi kuwa hatuna chochote cha kuogopa kutoka kwa shetani. Bwana wetu ametupa nguvu zote na mamlaka juu ya Shetani na vikosi vyake vya pepo: "Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru" ( Luka 10:19). Yesu anasema kwa wazi kwamba vita tunavyo pigana na Shetani tayari vishinda na tuna ndani yetu uwezo wa kupinga jaribio lolote na shetani linalo jaribu kutuangamiza.

Tuna migogoro na maadui wa kibinadamu wakati mwingine, watu tunaoishi au kufanya kazi pamoja. Pengine mtu amekuchokoza au kupinga sifa yako. Ugomvi unaosababisha dhiki kuu na huathiri afya yako ya kimwili.

Unaweza kumshtaki Bwana, "Nitaendelea kukusifu na kukuabudu, lakini usitarajie kwamba natatia chini hili." Lakini Bwana amesema waziwazi, "Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasmeheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi" (Waefeso 4:32). Na Yesu anasema, "Wapendeni adui zenu, nawabaariki wale wanaowalaani, fanyeni mema kwa wale wanaowachukia, na waombeeni wale wanaokutumia na kukutesa" (Mathayo 5:44).

Tunaleta utukufu kwa Baba yetu wa mbinguni wakati wowote tunaposubiri maumivu na kusamehe dhambi zilizofanyika kwetu. Tunaposamehe kama Mungu anavyosamehe, anatuleta katika ufunuo wa neema na baraka ambazo hatukuwahi kujua.