JIHADHARINI KWA KUJIAMINI KUPITA KIASI

David Wilkerson (1931-2011)

"Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniweke katika mimi, ili mpate kula na kunywa kwenye meza angu katika ufalme Wangu; na kuket kwenye viti vya enzi, huku kukiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli" (Luka 22: 29-30). Wafuasi wa Yesu walipaswa kusherehekea kusikia hii. Baadaye yao ilikuwa salama kabisa na Bwana mwenyewe alisema walielekea mbinguni ili kutawala na kutawala pamoja naye milele.

Kisha Yesu alizungumza na mtume Petro moja kwa moja: “'Simoni, Simoni, nisikilize! Shetani amewataka ninyi ili apate kuwapepeta kama vile ngano; Lakini, nimekuombea kwamba imani yako iwe na nguvu; nawe wakati utakapoongoka waimarishe ndugu zako. Petro akasema, Bwana, niko tayari kwenda nawe gerezani, na hata kufa nawe.Yesu akajibu, 'Petro, nakuambia, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui” (Luka 22:31-34).

Kujiamini sana, Petro hakujua ni nini angechokabiliana. Baadaye, kwenye Bustani ya Gethsemane, kwa kukamatwa kwa Yesu, alikata sikio la kulia la mtumwa wa kuhani mkuu (ona Yohana 18:10). Kitendo hiki cha ushujaa kilionyesha njia nyingi za Petro kwenye maisha. Na kabla ya usiku kumalizika alikuwa amekamilisha maneno ya Yesu kwamba angekataa mara tatu kwamba hata anamjua. Na "Petro akatoka nje, akalia kwa uchungu" (Luka 22:62).

Kutoka kwa kufurahishwa hadi ukiwa ndani ya muda wa masaa machache kwa sababu ya kujitegemea na kujiamini! Wakristo wengi wanaruhusiwa kuja mahali pakuanguka karibu ili Bwana aweze kuwainua na kuwaweka kwenye uwanja thabiti. Yesu alikuwa amemwambia Petro, "Utanikana, lakini utarejeshwa. Baadaye, utabarikiwa na yale umejifunza na utakuwa na kitu muhimu cha kuwapa wengine."

Mungu anakupenda bila masharti, na ana kusudi la milele kwako. Hata ingawa unaweza kupitia nyakati za kutofaulu, Shetani hawezi kukuibia upendo wa Kristo. "Kwa hiyo haturegeyi; bali ijapokuwa utu wetu wan je unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Kwa maana ziki yetu nyepesi, ambayo ni ya kitambo kidogo, inatutumikia uzani wa utukufu zaidi na wa milele" (2 Wakorintho 4:16-17).