JE! UNAKABILIWA NA SHIDA KUBWA?

David Wilkerson (1931-2011)

Ni rahisi kuchukua kwa kutowa nafasi ya miujiza ambayo Mungu ameifanya katika siku za nyuma. Hata hivyo Biblia inatuambia kukumbuka okovu wetu. Ushauri wa Musa kwa Israeli baada ya kufanyika muujiza wa Bahari Nyekundu ulikuwa, "Kumbukeni siku hii ambayo muliotoka nchini Misri, kutoka nyumba ya utumwa" (Kutoka 13:3).

Bwana alikuwa akiwaambia, kwa kweli, "Jihadharini kwa kumbukumbu hivyo na kila wakati unakabiliwa na mgogoro, kumbuka miujiza yote niliyokutolea. Na hakika kuwaambia watoto wako hivyo ili kujenga imani yako na imani ya kizazi kitachokufuata."

Kumbukumbu ya utoaji wetu wa zamani huongeza imani yetu kwa kile tunachokifanya sasa. Daudi alipojitolea kupigana na Goliathi mkuu, Mfalme Sauli akamwambia, "Huwezi wewe kumwendea Mfilisti huyu upigane naye; kwa maana wewe u kijana, naye ni mtu wa vita tangu ujana wake" (1 Samweli 17:33). Lakini Daudi alikuwa na kumbukumbu ya kuua simba na dubu kwa mikono yake wakati akiwalinda kondoo wake. Alimwambia Sauli juu ya hili na kumhakikishia, "Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyo Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai" (17:36).

Daudi alijua hatari ya kukabiliana na Goliathi, lakini hakuwa mwanafunzi katika kugombana, au kuwa mtoto mjinga, lakini mwenye ujasiri wa kuangalia mbele vita. Hapana, alikumbuka tu uokoaji wake wa zamani na kuhakikishiwa kushinda. Alimtazama adui wake kwa macho na akasema, "Bwana, ambaye aliniokowa kutoka kwenye makucha ya simba na makucha ya dubu, ataniokoa kutoka mkononi mwa Mfilisti huyu" (17:37).

Je! Unakabiliwa na shida kubwa katika maisha yako? Je!Unakumbuka wakati ambao Mungu aliponya mwili wako na kukuinua? Je! Unakumbuka wakati alipotoa fedha ambazo ulikuwa unahitaji kupata? Usiwe na hofu, lakini fikiria uaminifu wake na umwamini yeye akuokowe tena.